Page 73 - Fasihi_Kisw_F5
P. 73

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              kwa vijana kusimamia kile wanachokiamini. Mhusika Kalenga alisimama kidete
              kufichua uozo uliomo kwenye jamii, na hatimaye alipandishwa cheo kutokana na
              kazi nzuri aliyoifanya. Vilevile, kazi nyingine za fasihi kama nyimbo zimekuwa
              zikitumika kutia hamasa ya wanawake kufanya kazi ili kujiletea maendeleo bila
              kuwa wategemezi katika jamii.
          FOR ONLINE READING ONLY
              (g)  Kukosoa jamii
              Fasihi ina mchango katika kukosoa jamii kuhusiana na mambo mbalimbali ya
              maisha.  Kwa mfano,  katika  riwaya  ya  Kufikirika  (Robert,  1968), mwandishi
              anakosoa tabaka tawala  linalotumia  rasilimali  nyingi kwa manufaa  ya watu
              wachache  ilihali  wanajamii  wengine  wanateseka.  Halikadhalika,  methali
              katika fasihi hutumika kukosoa au kuonya jamii. Methali kama vile “Mkataa
              pema, pabaya panamwita” inakosoa mtu anayekataa wosia mzuri kwani kuna
              madhara yanaweza kumpata. Aidha, methali kama “Tamaa mbele, mauti nyuma”
              imekusudiwa kuwaonya wanajamii kuepuka tamaa kwani mtu mwenye tamaa
              anaweza kukabiliwa na madhara.

              (h)  Kukomboa jamii
              Fasihi simulizi na fasihi andishi imechangia sana kupiga vita masuala mbalimbali
              yanayokwamisha maendeleo ya jamii  kama vile  ujinga,  maradhi  na umaskini.
              Tamthiliya ya Hawala ya Fedha (Lihamba, 1985), kwa mfano, inaeleza mambo
              yanayosababisha umasikini ambayo ni ujinga na uvivu. Aidha, wakati wa harakati
              za ukombozi Kusini mwa Afrika, baadhi ya bendi za muziki wa dansi zilipiga
              nyimbo za kuwaunganisha watu kwa ajili ya ukombozi. Mfano mzuri wa wimbo
              wa “Mwenyekiti Mwalimu Nyerere” ulioimbwa na bendi ya Urafiki Jazz miaka
              ya 1970 wimbo huo ulikuwa ukimsihi mwenyekiti wa nchi tano zilizo mstari wa
              mbele kupigania ukombozi wa Kusini mwa Afrika azidishe mapambano kwani
              maadui wa Afrika walilisumbua sana Bara la Afrika.

               Shughuli ya 2.19

              (a)  Kwa kutumia vyanzo mbalimbali,  jadili  mchango wa fasihi andishi ya

                   Kiswahili katika jamii.
              (b)  Jadili uhusiano uliopo baina ya fasihi simulizi na fasihi andishi.

                Tamrini

                 1.   Kwa kutumia mifano, eleza namna sayansi na teknolojia zinavyochangia
                     katika kukuza fasihi simulizi na andishi.

                 2.   Fafanua tofauti kati ya maigizo na tamthiliya andishi ya Kiswahili.



                62                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   62
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   62                    23/06/2024   17:54
   68   69   70   71   72   73   74   75   76   77   78