Page 77 - Fasihi_Kisw_F5
P. 77

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Fani hufumbata maudhui; na maudhui ndiyo huitengeneza  au kuipa umbo
              fani. Inamaanisha kuwa ili kazi ya fasihi ikamilike na iwe bora, lazima iwe na
              vipengele vya fani na maudhui ambavyo huhitajiana, hushirikiana, hutegemeana,
              huwiana na hukamilishana.  Uwiano na ushirikiano wa fani na maudhui ndio
          FOR ONLINE READING ONLY
              unaokamilisha kazi ya fasihi.
               Shughuli ya 3.2

              (a)  Chambua vipengele vya fani  na  maudhui katika hadithi teule moja
                   uliyosoma kisha jibu maswali yafuatayo.

                   (i)  Ni kwa namna  gani  wahusika wa hadithi  hiyo wanahusiana  na
                        migogoro iliyojitokeza?

                   (ii)  Kwa nini mwandishi ametumia muundo alioutumia katika kufikisha
                        ujumbe wake?
                   (iii)  Ni kwa namna gani lugha iliyotumika  inachangia  kuibua maudhui
                        katika hadithi hiyo?

                   (iv)  Taswira alizozitumia mwandishi zina mchango gani katika kuelewa
                        dhamira za hadithi hii?

                   (v)  Mtindo wa uandishi wa hadithi hiyo umechangiaje katika kuwasilisha
                        maudhui?

              (b)  Chambua uhusiano wa fani na maudhui katika  kazi yoyote ya fasihi ya
                   Kiswahili.

              Uhusiano wa fani na maudhui katika kazi za fasihi
              Mwandishi na mhakiki wa kazi za fasihi anapaswa/hupaswa kuzingatia uhusiano
              wa vipengele vya fani na maudhui katika kubuni na kuchambua kazi. Endapo
              mwandishi na mhakiki huyo hatazingatia na kuhusianisha ipasavyo vipengele
              hivyo, vya fasihi uhakiki wake utakuwa chapwa.

               Shughuli ya 3.3
              Kwa kutumia mifano, jadili umuhimu wa fani na maudhui katika kazi za fasihi.



              Dhima za vipengele vya fani na maudhui katika kazi za fasihi
              Vipengele vya fani na maudhui vina dhima kubwa katika kazi ya fasihi. Dhima
              hizo muhimu zinaweza kuelezwa kama ifuatavyo:




                66                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   66
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   66                    23/06/2024   17:54
   72   73   74   75   76   77   78   79   80   81   82