Page 80 - Fasihi_Kisw_F5
P. 80

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              (iii)  kumsaidia  mhakiki  kugundua jambo  jipya  au kuliboresha  lililokuwapo
                   awali.

              Uchambuzi wa nadharia teule za uhakiki wa kazi za fasihi
          FOR ONLINE READING ONLY
               Shughuli ya 3.5
              Kwa kutumia  vyanzo vya mtandaoni  au maktabani, taja nadharia  nne (4) za
              uhakiki wa kazi za fasihi.

               Shughuli ya 3.6
              Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni au maktabani, fafanua maana na misingi ya
              nadharia ya umuundo katika kuhakiki kazi za fasihi.


              Nadharia ya umuundo
              Umuundo ni nadharia ya uhakiki wa fasihi iliyojikita kwenye taratibu zilizopo
              katika  uundwaji  wa kazi  ya  kifasihi.  Miongoni  mwa  waasisi  wa nadharia  hii
              ni Ferdinand de Saussure (1857-1913) aliyeanzisha  umuundo wa kiisimu.
              Wanamuundo wanaeleza kuwa lugha ni mfumo wa ishara nasibu, na kwamba
              kila kipengele kinahusiana na vipengele vingine katika mfumo huo. Kama ilivyo
              katika mfumo wa lugha, fasihi nayo imeundwa na vipengele vinavyotegemeana.
              Katika kazi ya fasihi kuna vipengele vya kisanaa vinavyojidhihirisha katika fani na
              maudhui. Vipengele hivyo huelezwa kwa kutegemeana, kwani hakuna kipengele
              kinachoweza  kusimama  peke  yake  bila  kuhusishwa na kingine.  Nadharia
              ya  umuundo huonesha  namna  vipengele  vya  kazi  ya  fasihi  vinavyohusiana
              na kufungamana  hadi  kuikamilisha  kazi  husika. Kwa jumla,  wanaumuundo
              wanaeleza kuwa kazi ya fasihi haina urejelezi wa nje bali huonwa kama mfumo
              unaojitosheleza.

              Misingi ya nadharia ya umuundo
              Misingi mikuu ya nadharia ya umuundo ni:

              (i)  lugha  hutawaliwa  na  mfumo wa ishara,  ambapo  vipengele  vinavyounda
                   mfumo huo huweza kueleweka tu kwa kuangalia uhusiano wake na
                   vipengele vingine katika mfumo huo wa lugha badala ya kuangalia nje ya
                   mfumo wa lugha husika;

              (ii)  maana ya fasihi imejificha ndani ya mfumo wa lugha;

              (iii)  ishara haielezi wala haitoi uhusiano baina ya neno na kitu, bali ni
                   muunganiko changamani kati ya dhana iliyopo akilini na ruwaza za sauti
                   zinazoendana na dhana hiyo; na


                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            69
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   69                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   69
   75   76   77   78   79   80   81   82   83   84   85