Page 81 - Fasihi_Kisw_F5
P. 81

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Katika kuchambua kazi ya fasihi kwa kutumia nadharia ya umuundo, unatakiwa
              kuchunguza  matumizi  ya  lugha,  na  uhusiano  wa  vipengele  vya  lugha  katika
              kutoa maana ya kazi hiyo. Pia, chunguza namna wahusika wanavyoitumia
              lugha kufikisha ujumbe uliokusudiwa. Vilevile, chunguza jinsi taswira na ishara
          FOR ONLINE READING ONLY
              mbalimbali  zilivyotumika  kujenga maana ya kazi hiyo ya fasihi. Kadhalika,
              fafanua mpangilio wa vipengele vya kazi hiyo. Mathalani, iwapo unachambua
              shairi zingatia  namna vina, mizani, vibwagizo, beti, na mpangilio  kwa jumla
              vinavyosaidia kupatikana kwa maana ya shairi.

               Shughuli ya 3.7
              Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni au maktabani, fafanua maana na misingi ya
              nadharia ya umaksi katika kuhakiki kazi za fasihi.

              Nadharia ya umaksi
              Umaksi ni nadharia inayozungumzia harakati za mwanadamu katika kupambana
              na utabaka uliomo katika jamii yake. Harakati hizo huhusiana na masuala ya
              uchumi, historia, siasa, jamii na mapinduzi, ambapo tabaka linalodhibiti njia kuu
              za uzalishaji mali huitawala na kuidhibiti jamii. Nadharia hii iliasisiwa na Karl
              Marx (1818 - 1883) na Friedrich Engels (1820 - 1895) kupitia kazi zao za Das
              Kapital (1867) na Communist Manifesto (1848). Jambo kubwa katika nadharia
              hii siyo kuufasili ulimwengu tu, bali kuubadilisha. Kwa mujibu wa Karl Marx,
              tabaka moja hutoweka na lingine huchipuka kwa sababu ya mgongano unaotokea
              kati ya tabaka tawala na tabaka tawaliwa. Mgongano huo hutokea kwa sababu
              kila mara kuna tabaka la wanyonyaji na wanyonywaji.

              Kwa jumla, nadharia ya umaksi huhusisha kazi za fasihi na uhalisi wa kijamii wa
              wakati kazi hizo zilipotungwa. Vilevile, nadharia hii huzingatia zaidi maudhui
              katika uhakiki wa kazi za kifasihi huku ikijikita katika kuhakiki maadili na njia
              za kuyaboresha maisha.

              Misingi ya nadharia ya umaksi
              Nadharia ya umaksi ina misingi mbalimbali inayotumika katika uhakiki wa kazi
              za kifasihi. Misingi hiyo ni:

                   (i)  kutumia  historia  ya binadamu  kuakisi  harakati za kitabaka
                        zinazoendelea katika jamii;

                   (ii)  kuvunjiliwa mbali kwa ubepari kama njia ya uzalishaji mali kutokana
                        na jitihada mbalimbali za kitabaka za kuuangamiza;





                70                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   70
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   70                    23/06/2024   17:54
   76   77   78   79   80   81   82   83   84   85   86