Page 86 - Fasihi_Kisw_F5
P. 86

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




               Shughuli ya 3.11
              Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni na maktabani, fafanua maana na misingi ya
              nadharia ya mwingilianomatini katika kuhakiki kazi za fasihi.

              Nadharia ya mwingilianomatini
          FOR ONLINE READING ONLY
              Nadharia ya mwingilianomatini inahusu namna matini moja inavyohusiana na
              matini nyingine. Kwa jumla, nadharia hii husisitiza kwamba kila kazi ya kifasihi
              kwa namna moja au nyingine inahusiana na kazi iliyoandikwa kabla au kazi
              nyingine mbalimbali. Katika uhusiano huo, vipengele vya kifani na kimaudhui
              vya kazi moja ya mwanzo huathiri kazi mpya kwa namna ambayo huonesha
              kufanana kwa vipengele vya kazi hizo.


              Nadharia ya mwingilianomatini iliasisiwa na Julia Kristeva (1941 hadi sasa)
              kutokana na mawazo aliyoyapata katika nadharia ya usemezano iliyoasisiwa na
              Mikhail Bakhtin (1895-1975). Kristeva anaitazama dhana ya mwingilianomatini
              kama jumla ya maarifa na mbinu zinazoifanya maana ya matini moja kueleweka
              kwa kuhusisha na matini nyingine.

              Misingi ya nadharia ya mwingilianomatini
              Ifuatayo ni misingi ya nadharia ya mwingilianomatini:


              (i)  hakuna matini inayoweza kuchunguzwa peke yake kwa kujitegemea, bali
                   lazima pawe na matini nyingine iliyotangulia inayohusiana na matini hiyo
                   mpya;

              (ii)  matini  za kifasihi huchota, hunukuu, hugeuza, na kuiga kwa namna ya
                   kubeza au kurejelea kwa njia moja au nyingine; na
              (iii)  kazi za kifasihi huundwa kutokana na tamaduni mbalimbali zinazopatikana
                   katika matini mbalimbali za kifasihi na zisizo za kifasihi.

              Kwa hiyo, unapohakiki kazi ya fasihi kwa kutumia nadharia ya mwingilianomatini
              unatakiwa kuangalia uhusiano wa matini moja na matini nyingine kwa kutumia
              ulinganishi wa vipengele vya kifani na kimaudhui katika kazi mpya na zile za
              awali. Kwa mfano, unaweza kuchunguza namna wahusika walivyochorwa, jinsi
              mandhari yanavyoathiri tabia na matukio katika kazi ya fasihi, matukio mbalimbali
              ya kihistoria, mtindo na mbinu za uandishi, mwingiliano wa kiutamaduni, na
              uwasilishwaji wa maudhui. Pia, unaweza kuchunguza mwingiliano  wa fasihi
              simulizi na andishi, mwingiliano wa tanzu, na mwingiliano wa vipera.






                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            75
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   75                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   75
   81   82   83   84   85   86   87   88   89   90   91