Page 87 - Fasihi_Kisw_F5
P. 87

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Mpaka hapa umejifunza baadhi ya nadharia muhimu zinazotumika katika uhakiki
              wa kazi za fasihi. Nadharia hizi zitakupa  mwongozo katika  kuchambua kazi
              mbalimbali za kifasihi.


               Shughuli ya 3.12
          FOR ONLINE READING ONLY
              Kwa kutumia  vyanzo  vya mtandaoni  na  maktabani,  eleza  sifa  na  dhima  za
              mhakiki wa kazi za kifasihi.

              Kuhakiki kazi za fasihi kwa kutumia nadharia za kifasihi
              Taaluma ya uhakiki ilianza zamani, tangu enzi za mwanafalsafa wa zamani wa
              Kiyunani, Plato, (takribani miaka ya 428 - 348 K.K). Nchini Tanzania, taaluma
              hii ilianza kutumika zaidi miaka ya 1970 baada ya baadhi ya Watanzania kusoma
              taaluma  ya fasihi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Miongoni mwao
              walikuwa John Ramadhani, May Balisidya, Saifu Kiango, Euphrase Kezilahabi,
              na Mbunda Msokile. Wengine ni pamoja na Farouk Topan, Tigiti Sengo, Fikeni
              Senkoro na Mugyabuso Mulokozi.


              Unapohakiki  kazi  ya fasihi unachambua  na kutathmini  mawazo  au masuala
              mbalimbali yaliyomo katika kazi hiyo. Mbali na kuwa na maarifa ya nadharia
              zinazoongoza  katika kuchambua kazi za fasihi, unapaswa kufahamu historia
              na siasa ya jamii inayohusika ili uweze kuelewa masuala muhimu katika jamii
              husika.  Halikadhalika,  inakulazimu  kusoma  kazi  nyingine  za  fasihi  tofauti
              na ile unayoihakiki ili uwe na ujuzi zaidi katika uwanja wa uhakiki. Vilevile,
              unapohakiki kazi za fasihi ni muhimu kujua historia na mazingira yaliyomkuza
              mwandishi au msanii; na mwisho kueleza bayana ubora na upungufu wa kazi
              husika.


              Ukiwa na ufahamu wa kutosha kuhusu nadharia,  itakuwia  rahisi kuamua ni
              nadharia gani uitumie katika kuhakiki kazi fulani ya fasihi. Uteuzi wa nadharia
              ya kutumika hutegemea mwelekeo wa jumla wa kazi inayohakikiwa pamoja na
              kipengele au vipengele mahususi unavyotaka kuvifanyia uhakiki.

              Kumekuwa na mjadala kuhusu nafasi ya mhakiki wa kazi za fasihi. Mjadala huu
              umetokana  na kuwapo kwa mitazamo  miwili inayopingana  kuhusu nafasi ya
              mhakiki huyo. Mtazamo wa kwanza unaona kwamba msanii na mhakiki ni watu
              ambao wanahitajiana kwa sababu mhakiki ndiye anayeieleza na kuitambulisha
              kazi ya msanii kwa hadhira.  Vilevile,  mhakiki  ndiye anayemtahadharisha
              mwandishi kuhusu makosa aliyoyafanya ndani ya kazi yake na kumfanya awe
              makini  zaidi  katika  kushughulikia  kazi  nyingine.  Aidha, mhakiki  ni kiungo
              muhimu kati ya jamii na msanii kwa sababu hutumia ujuzi wake wa kuchambua


                76                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   76
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   76                    23/06/2024   17:54
   82   83   84   85   86   87   88   89   90   91   92