Page 89 - Fasihi_Kisw_F5
P. 89

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                 3.   Linganisha  nadharia  za  umuundo na umaksi  zinavyotumika  katika
                     uchambuzi wa kazi za fasihi.

                 4.   Fafanua tofauti zilizopo  kati ya nadharia ya mwingilianomatini  na
                     mwitiko wa msomaji.
          FOR ONLINE READING ONLY
                 5.   Eleza tofauti zilizopo kati ya nadharia ya ufeministi na uhalisia.

                 6.   Mhakiki hana nafasi katika kazi za fasihi. Jadili.

                 7.   Kwa kutumia mifano, fafanua mitazamo kuhusu mhakiki wa kazi ya
                     fasihi kisha toa maoni yako.



              Kuhakiki maigizo, mashairi, na tamthiliya kwa kutumia nadharia za kifasihi
              Uchambuzi wa kazi za fasihi kwa kutumia nadharia za kifasihi huzingatia misingi
              ya uhakiki ya nadharia husika. Hivyo, mhakiki anapaswa kuzingatia misingi ya
              kila nadharia katika kuhakiki kazi za kifasihi. Ufuatao ni ufafanuzi wa namna ya
              kuhakiki maigizo, mashairi na tamthiliya kwa kutumia nadharia za kifasihi.


              Kuhakiki maigizo kwa kutumia nadharia za kifasihi
               Shughuli ya 3.13

              (a)  Tazama igizo katika runinga au vifaa vingine vya TEHAMA, kisha hakiki
                   igizo hilo kwa kutumia nadharia ya uhalisia, huku ukiongozwa na maswali

                   yafuatayo:
                   (i)  Ni kwa namna gani maudhui yaliyowasilishwa na wahusika katika
                        maigizo hayo yanaakisi hali halisi katika jamii?

                   (ii)  Ni kwa namna gani uumbaji wa wahusika katika maigizo hayo unaakisi
                        hali halisi?
                   (iii)  Maudhui yanayowasilishwa katika maigizo hayo yana athari gani kwa
                        jamii?

                   (iv)  Je, lugha ya wahusika katika maigizo hayo ina uhalisi?

                   (v)  Ni kwa namna gani mandhari ya maigizo hayo yanasawiri mazingira
                        halisi?








                78                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   78                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   78
   84   85   86   87   88   89   90   91   92   93   94