Page 84 - Fasihi_Kisw_F5
P. 84

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Kwa hiyo, unapohakiki  kazi ya fasihi kwa kutumia  nadharia  ya ufeministi,
              unatakiwa  kuchambua  masuala  yanayohusiana  na usawa wa kijinsia  kati  ya
              mwanamke na mwanamume katika  nyanja za kiutamaduni,  kidini, kijamii,
              kisiasa, na kiuchumi.
          FOR ONLINE READING ONLY
               Shughuli ya 3.9
              Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni na maktabani, fafanua maana na misingi ya
              nadharia ya uhalisia katika kuhakiki kazi za fasihi.

              Nadharia ya uhalisia
              Nadharia ya uhalisia  inahusu kusawiri na kuakisi maisha ya mwanadamu  na
              mazingira. Nadharia hii inaepuka masuala ya unjozi na huyaelezea maisha kwa
              uyakinifu kama yalivyo katika jamii. Waasisi wa nadharia hii ni: George Wilhelm
              Hegel (1770-1831), Friedrich Schiller (1759-1805), na Gustave Flaubert (1821-
              1880). Nadharia hii husisitiza kuwa kazi ya sanaa ioneshe maisha ya binadamu
              jinsi  yalivyo.  Kimsingi,  nadharia  hii  inaichukulia  kazi  ya  fasihi  kama  kioo
              kinachoonesha masuala mbalimbali yanayohusiana na maisha ya binadamu.

              Misingi ya nadharia ya uhalisia

              Ifuatayo ni misingi ya nadharia ya uhalisia ni:

              (i)  uwasilishaji wa maudhui ya kazi ya fasihi uzingatie hali halisi ya jamii;

              (ii)  mandhari ya kazi ya fasihi yaakisi mazingira halisi;
              (iii)  wahusika wasawiriwe kiyakinifu ili kuakisi maisha ya kila siku;

              (iv)  matukio katika kazi ya fasihi yaakisi mambo kama yalivyo kisiasa, kiuchumi,
                   na kutamaduni na kijamii;

              (v)  changamoto za kijamii zitatuliwe kwa njia zinazothibitika kisayansi; na
              (vi)  lugha inayotumika kwenye kazi za fasihi iwe ile inayoeleweka kwa msomaji/
                   hadhira lengwa.

              Unapohakiki kazi ya fasihi kwa kutumia nadharia ya uhalisia, unatakiwa
              kuchunguza namna mwandishi alivyowaumba na kuwasawiri wahusika,
              matumizi ya lugha ya kawaida, namna matukio yanavyoakisi hali halisi, na
              jinsi mandhari ilivyochorwa.  Vilevile, hakiki namna maudhui ya kazi hiyo
              yanavyoakisi hali halisi na ukweli wa maisha ya jamii husika.







                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            73
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   73                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   73
   79   80   81   82   83   84   85   86   87   88   89