Page 83 - Fasihi_Kisw_F5
P. 83

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Steady (1981) ni miongoni mwa waasisi wa nadharia ya ufeministi wa Kiafrika.
              Huyu alitumia  nadharia  hii  kubainisha  dhuluma  zilizokuwa  zikimkandamiza
              mwanamke wa Kiafrika kama vile kutokuwa na uhuru wa kuchagua kuwa mzazi
              kwa wakati gani au kujichagulia mume; ukeketaji wa mwanamke, unyamavu
          FOR ONLINE READING ONLY
              wa kulazimishwa, urithi wa mali, mila za kurithiwa, rangi yake mwenyewe na
              kubaguliwa kwa mwamwake tasa.

              Katika kutahadharisha kuhusu ufeministi,  Badru (2019) anaeleza  kuwa tangu
              kuanza kwa mawazo ya ufeministi ulimwenguni msisitizo mkubwa umekuwa
              ni namna gani wanawake wanaweza kujikomboa kwa kubadilisha mfumo-dume
              na kupata haki na wajibu sawa. Pamoja na hatua kubwa iliyopigwa, mapigano
              haya hayawezi kufanikiwa iwapo yatakuwa mapigano ya wanawake dhidi ya
              wanaume. Iwapo mwanaume ataachwa nyuma na asikombolewe kutoka katika
              ufungwa  wa  kifikra,  kiutamaduni  na  kiuchumi  alimofungwa  hakuna  namna
              ambavyo mapambano haya yatafanikiwa.


              Ni vizuri kujua kuwa nadharia ya ufeministi wa Kiafrika hainuii kuleta mgogoro
              na mvutano wa nafasi mbalimbali baina ya mwanamume na mwanamke katika
              jamii; bali unalenga kuamsha uelewa na usawa baina yao.

              Misingi ya nadharia ya ufeministi
              Ifuatayo ni misingi ya nadharia ya ufeministi ni:

              (i)  kukuza na kuendeleza umoja wa wanawake kupitia majukwaa mbalimbali;

              (ii)  kuleta  usawa wa kijinsia katika  maeneo  mbalimbali  kama  malezi  na
                   mgawanyo wa majukumu;

              (iii)  kumpa mwanamke uhuru na nguvu ya kufanya maamuzi katika jamii;
              (iv)  kuelezea kwa undani hali ya mwanamke ili kumsaidia mtu yeyote kuielewa
                   hali hiyo;

              (v)  kumpa mwanamke haki ya kushirikishwa na kushiriki  katika  masuala
                   mbalimbali ya jamii;

              (vi)  kuhimiza mhusika wa kike katika kazi za fasihi awe mfano mzuri wa kuigwa
                   katika jamii;
              (vii) kutambua na kuthamini kazi za fasihi zilizotungwa na wanawake; na

              (viii) kuepuka usaguzi wa kimapokeo uliojengewa misingi ya kiimani na wenye
                   mawazo hasi kuhusu nafasi ya mwanamke katika jamii.



                72                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   72                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   72
   78   79   80   81   82   83   84   85   86   87   88