Page 79 - Fasihi_Kisw_F5
P. 79

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari





                 3.   “Fani na maudhui ni kama pande mbili za sarafu.” Jadili kauli hii.

                 4.   Eleza ubora na udhaifu wa mitazamo ya kidhanifu na kiyakinifu katika
                     kutoa maana ya fani na maudhui.
          FOR ONLINE READING ONLY

              Nadharia za uhakiki wa kazi za fasihi

               Shughuli ya 3.4
              Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni na maktabani, eleza maana, sifa na umuhimu
              wa nadharia za uhakiki.

              Dhana ya nadharia na nadharia ya uhakiki
              Wataalamu mbalimbali kama vile Massamba na wenzake (2009) na Mulokozi
              (2017) wanakubaliana  kuwa nadharia ni utaratibu  au mwongozo unaosaidia
              kueleza jambo fulani. Kwa msingi wa fasili hii, nadharia ya uhakiki ni mwongozo
              unaoelekeza namna ya kufafanua vipengele vya fani na maudhui ya kazi za fasihi.


              Kwa muktadha wa kifasihi, Wafula na Njogu (2013) wanasema kwamba nadharia
              za uhakiki ni miongozo inayomwelekeza msomaji wa kazi ya fasihi kuifahamu
              kazi hiyo na vipengele vyake. Hivyo, nadharia za uhakiki wa kazi za fasihi ni
              mawazo,  maelezo  au  miongozo  iliyopangwa  ili  kusaidia  kufafanua  vipengele
              mbalimbali vya kazi hizo.

              Sifa za nadharia za uhakiki wa kazi za fasihi
              Nadharia za uhakiki huwa na sifa zifuatazo:

              (i)  kuwa na malengo mahususi yanayokusudiwa kutimizwa;

              (ii)  kuwa na misingi mikuu ambayo ni mwongozo wa uchambuzi au uhakiki; na
              (iii)  kuwa na mpangilio inayojengana na kukamilishana katika kufafanua mambo
                   yanayopatikana katika kazi husika.

              Umuhimu wa nadharia za uhakiki wa kazi za fasihi
              Nadharia za uhakiki zina umuhimu ufuatao:


              (i)  kumwongoza mhakiki katika uchambuzi na uhakiki wa kazi za fasihi kupitia
                   misingi na maudhui yake makuu;

              (ii)  kumsaidia mhakiki kuzielewa na kuzitumia nadharia mbalimbali za fasihi;
                   na




                68                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   68
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   68                    23/06/2024   17:54
   74   75   76   77   78   79   80   81   82   83   84