Page 92 - Fasihi_Kisw_F5
P. 92

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




               Shughuli ya 3.15

              (a)  Hakiki mashairi mawili kutoka katika diwani teule kwa kutumia nadharia
                   ya umuundo.
          FOR ONLINE READING ONLY
              (b)  Soma shairi lifuatalo, kisha hakiki kwa kutumia nadharia ya ufeministi kwa
                   kujibu maswali yafuatayo.


                                Maisha ya Ndoa

                                Mume
                                Nimeagiza chakula, wanisogezea uji,
                                Nikiangalia saa, ni mwanana adhuhuri,

                                Ni ya msosi majira, umenitengea nini?

                                Haya maisha ya ndoa, wenzangu mnaishije?

                                Mke
                                Mboga unga na mkaa, mwenzangu mi’ sivioni,

                                Nimechoka kulalama, mapenzio siyaoni?


                                Unazicheza karata, pesa zako sizioni,
                                Haya maisha ya ndoa, wenzangu mnaishije?


                                Mume
                                Wewe mke sikiliza, tena usiwe shubiri,

                                Makonzi nitakutia, mke gani we bilisi!
                                Umepuya huna uja, hatari bora ya chui,

                                Haya maisha ya ndoa, mwenzangu mnaishije?

                                Mke

                                Mume tega masikia, nisikize kwa makini,
                                Majukumu nayajua, jikoni hadi chumbani,

                                Kuchapana zilipendwa, ndoa sio utumwani,

                                Haya maisha ya ndoa, wenzangu mnaishije?




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            81
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   81                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   81
   87   88   89   90   91   92   93   94   95   96   97