Page 97 - Fasihi_Kisw_F5
P. 97

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                                  Ben peke yake ndiye aliyekuwa  na mimi. Jamaa za mume
                                wangu vilevile, walimtenga siku hiyohiyo ya ndoa. Lakini
                                nikaona si kitu tutaishi.  Mimi, wewe, Herbert. Kwa nini
                                isiwezekane  ikiwa pendo lipo?  Kwa nini  tusiweze?  Lakini
          FOR ONLINE READING ONLY
                                hata hi…
                   Chris:       Ma!

                                (Kimya, Mtu anagonga mlango)

                   Martha:      Mtazame nani.

                                (Ingia George)

                   George:      Habari Martha.

                                (Martha hajibu)
                                A-a! Chris

                                (Chris hajibu. Baada ya muda)


                   George:      Nimekuja kuchukua hati.

                   Martha:      Hati?

                   George:      Tunataka kuchukua maiti kutoka hospitali.

                                (Kimya)

                   Martha:       Sina hati. Sisi tutamzika  hapa. Nimeshamwomba Pasta
                                atatusaidia kumzika. Tumewaambia marafiki zetu watakuja.
                                Na wewe…

                   George:      Utamzika wapi?

                   Martha:      Hapa! Pale.

                                (Anaonesha nje ya dirisha)

                   George::     Ndivyo alivyousia marehemu?

                   Martha:      Ndiyo.

                   George:      Hakikisha.

                   Martha:      Usinifokee. Kama unataka kufoka nenda nyumbani kwako.


                86                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   86
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   86                    23/06/2024   17:54
   92   93   94   95   96   97   98   99   100   101   102