Page 98 - Fasihi_Kisw_F5
P. 98

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                   George:      Bado haujaelewa. Ninyi mko ndani ya madaraka yangu.

                   Martha:      Nini?

                   George:      Mko chini…
          FOR ONLINE READING ONLY
                   Martha:       Katika  nyumba hii wewe huna madaraka yoyote!  Tena
                                tafadhali ondoka.

                   George:      Ond …


                                (Hakudhani kuwa Martha atasema hivyo)

                                Unajua unasema nini?

                   Martha:      Nasema nini?

                   George:       Labda huelewi. Herbert hakukueleza. Kimila, mimi ni mkubwa
                                wa Herbert. Mama yangu aliolewa, halafu mama aliyemzaa
                                Herbert.


                                    Kwenye Ukingo wa Thim (Hussein, 2004: 24 - 28)
              Maswali
                   (i)  Mgogoro kati ya Martha na George unatokana na nini?

                   (ii)  Kuna uhusiano gani kati ya mambo yanayosawiriwa katika kipande
                        hiki cha tamthiliya na jamii yako?

                   (iii)  Kutokana na matini  hii, ni kwa namna gani mwandishi anasawiri
                        matabaka na mifumo mbalimbali ya maisha katika jamii yako?

                   (iv)  Jamii inapaswa kufanya nini ili kuepusha migogoro kama
                        inavyosawiriwa katika matini hii?
                   (v)  Kwa namna gani matini hii imesawiri upiganiaji wa haki na suluhu
                        yake?

                   (vi)  Utamaduni umeathirije maisha ya familia ya Herbert na Martha katika
                        matini hii?

              (b)  Hakiki tamthiliya moja teule kwa kutumia nadharia ya umaksi.

              (c)  Hakiki tamthiliya moja teule kwa kutumia nadharia ya mwingilianomatini.




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            87
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   87                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   87
   93   94   95   96   97   98   99   100   101   102   103