Page 102 - Fasihi_Kisw_F5
P. 102

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari






                    Sura

                      ya                     Maadili katika fasihi
          FOR ONLINE READING ONLY
                     Nne






                          Utangulizi

               Maadili katika kazi za fasihi ni muhimu kwani husaidia kujenga mwenendo
               na tabia inayokubalika katika jamii. Hivyo, kazi za fasihi zimekuwa chachu

               ya kubadilisha jamii kupitia ujumbe unaopatikana katika kazi hizo. Katika
               sura hii, utajifunza maadili yaliyomo katika nyimbo za bongo fleva, mashairi,
               na tamthiliya. Pia, utajifunza misingi ya maadili, umuhimu wa maadili katika
               jamii na maadili  yaliyosawiriwa  katika  kazi za fasihi. Vilevile,  utajifunza
               namna ya kueleza na kuhusianisha mitazamo iliyomo katika kazi hizo za fasihi
               na matendo ya jamii  na athari za kiimani  na kimtazamo zinavyodhihirika
               katika  jamii. Umahiri utakaoupata katika  sura hii utakuwezesha kutunga

               kazi za fasihi zenye kujenga maadili kulingana na mtazamo na imani ya jamii
               husika.





                            Kazi za fasihi zinavyochochea  ujenzi wa maadili katika
                            jamii


              Maadili katika nyimbo za bongo fleva, mashairi na tamthiliya

               Shughuli ya 4.1

              Sikiliza  au  tazama  nyimbo  za  bongo  fleva  kisha  bainisha  wimbo  mmoja
              unaodhani una maadili na wimbo mwingine unaodhani hauna maadili na eleza
              kwa nini unasema wimbo fulani umezingatia maadili au la.

              Maadili ni nini?
              Maadili ni kanuni, miongozo na taratibu zilizowekwa na jamii ili kusimamia
              mienendo na tabia za watu zinazokubalika katika jamii husika. Maadili huathiri


                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            91
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   91                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   91
   97   98   99   100   101   102   103   104   105   106   107