Page 106 - Fasihi_Kisw_F5
P. 106

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                             Hupendezwa kiongoke, cha kwake au cha kwetu,
                             Hupendezwa moyo wake, usitekwe mji wetu,

                             Japokuwa muudhike, yeye haogopi kitu,
          FOR ONLINE READING ONLY
                             Shujaa haogopi kitu, kilicho halali yake.




                             Hodari nyumbani kwake, huwakaribisha watu,
                             Hutetea nchi yake, asiichafue mtu,

                             Yu tayari peke yake, kuutembelea mwitu,

                             Shujaa haogopi kitu, kilicho halali yake.

                                    Mashairi ya Saadani (Kandoro, 1972:66)

                   Maswali

                   (i)  Ni dhamira gani zinazopatikana katika shairi hili?

                   (ii)  Kutokana na shairi ulilolisoma, unafikiri ni kwa namna gani maadili
                        yaliyomo yanaakisi jamii yako?

                   (iii)  Ni kwa namna gani jina la shairi linaakisi maadili?
                   (iv)  Unafikiri lugha iliyotumika inasawiri maadili ya jamii? Kwa nini?

                   (v)  Mwandishi anamaanisha  nini anaposema “Hodari kwa haki yake,
                        hapendi ipate kutu”?

                   (vi)  Ni kwa namna gani mbinu za kisanaa zinaibua maadili katika shairi
                        hili?
                   (vii) Una mtazamo gani kuhusu maadili yanayoelezwa katika shairi hili?


              (b)  Chambua maadili yaliyomo katika mashairi mawili uliyosoma katika
                   diwani teule.

              Maadili katika tamthiliya
              Kutokana na kusoma au kutazama tamthiliya katika runinga, watu wamekuwa
              wakijifunza mambo mengi yanayotokea au ambayo hayajapata kutokea katika
              jamii  zetu.  Haya  yote  yanatoa  mafundisho  yenye  kuadilisha  kutoka  katika
              tamthiliya hizo na kuyaendeleza kwa manufaa ya jamii nzima.




                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            95
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   95                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   95
   101   102   103   104   105   106   107   108   109   110   111