Page 108 - Fasihi_Kisw_F5
P. 108

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                   Ngahinyana:       (Huku akicheka): Ehe ... Ehee ... Wazee wakati mwingine
                                    huwa tuna hasira. Kuna barua yetu? Kutoka Dalisalaam?

                   Pata:              Nadhani inatoka Dar es Salaam. (Anapekuapekua barua
          FOR ONLINE READING ONLY
                                    hatimaye anaipata).  Hii hapa. Haya mzee nakwenda.

                   Ngahinyana:       Asante sana. Pole sana kwa kukupiga;  nisamehe
                                    mwanangu.

                   Pata:              Si kitu mzee. (Anatoka) Siku nyingine usinivizie nyuma ya
                                    mlango. Ningoje tuonane macho kwa macho. (Anatoka)

                   Mama Huka:     (Anacheka): Hee ... he ... he ... Ooiii! Unaona sasa,
                                    nilikuambia  mimi. Umempiga mtoto wa watu bure.
                                    Atapita kusema kila mahali.


                   Ngahinyana:      Basi na wewe ... (Anachana barua na kuisoma.)

                   Mama Huka:       Inatoka kwa shemeji?


                   Ngahinyana:      Ee! Anashtuka na kutoa macho). Mh!

                   Mama Huka:       Nini (Anamsogelea.)


                   Ngahinyana:       Mh, (Huku akitikisa kichwa). Sikiliza. (Anasoma.) Kwa
                                    kaka mpenzi,

                                      Natum... ma... ininy... temu wa... zi... makusu...dihasa...

                                      la...ku...waa... ndi... kiani... kuwa... aa... ri...fuma.. mbo..
                                    fu.. lani...  kuhu.. Huka. (Anaendelea  kusoma hivyo
                                    akikwamakwama). Kwanza hakuchaguliwa kuendelea na
                                    shule. Pia, Huka, nasikitika, kuwaeleza, kuwa amebomoa
                                    nyumba ya watu. Nina maana amewagombanisha  Bi.
                                    na Bwana Kambanga  hata  wameachana.  (Anaachia
                                    hapo.  Anamwelekea  Mama Huka). Unaona jinsi
                                    mwanao  anavyofanya.  Tulikuwa  tukisema  sasa hivi.
                                    (Anageuka kumwita Huka).  Unaona,  alipofika  yule






                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            97
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   97                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   97
   103   104   105   106   107   108   109   110   111   112   113