Page 105 - Fasihi_Kisw_F5
P. 105

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




               Shughuli ya 4.2

              (a)  Kwa kutumia vyanzo vya mkondoni na vinginevyo, sikiliza wimbo wowote
                   wa bongo fleva unaosawiri umuhimu wa wazazi, au kusisitiza kazi au utu
                   wema kisha jibu maswali yafuatayo.
          FOR ONLINE READING ONLY
                   (i)  Ni dhamira zipi zinazopatikana katika wimbo huo?

                   (ii)  Ni maadili gani yanayopatikana katika wimbo huo? (toa mifano)
                   (iii)  Una mtazamo gani kuhusu wimbo huo?

                   (iv)  Lugha iliyotumika katika wimbo huo inasawiri vipi suala la maadili?
                   (v)  Wimbo huo una mchango gani katika kuhamasisha maadili ya jamii
                        ya Tanzania?

              (b)  Kwa kutumia vyanzo vya mtandaoni na vinginevyo, sikiliza nyimbo mbili

                   za bongo fleva, kisha chambua maadili yaliyomo katika nyimbo hizo.
              Maadili katika mashairi
              Waandishi  wengi  wamekuwa wakitunga  mashairi  yenye  maudhui  mbalimbali
              yanayoshughulikia masuala ya kijamii. Mashairi yana mchango mkubwa katika
              kutoa maadili mbalimbali yanayoelimisha na kuburudisha jamii.

               Shughuli ya 4.3

              (a)  Chambua maadili yaliyomo katika shairi hili huku ukiongozwa na maswali
                   yanayofuata.



                         Shujaa haogopi kitu kilicho halali yake
                         Nisemayo muyashike, hili ni shairi letu,

                         Akuitae muitike, tuendeshe mambo yetu,
                         Shujaa na kitu chake, hadhulumiwi na mtu.
                         Shujaa hahofu kitu, kilicho halali yake.


                         Hodari kwa haki yake, hapendi ipate kutu,

                         Tena hageuki ike, japokuwa mwana kwetu,
                         Japo mtoto mshike, atafanya utukutu,

                         Shujaa haogopi kitu, kilicho halali yake.




                94                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   94                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   94
   100   101   102   103   104   105   106   107   108   109   110