Page 110 - Fasihi_Kisw_F5
P. 110

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Ulinganisho wa maadili na imani katika bongo fleva
              Kwa upande wa fasihi, nyimbo nyingi za bongo fleva zimetumika kubeba maadili
              yanayoendana na imani zilizopo katika jamii ya Watanzania ijapokuwa baadhi ya
              nyimbo hizo zimekuwa zikikiuka maadili hayo na kasababisha kufungiwa.
          FOR ONLINE READING ONLY
               Shughuli ya 4.6

              (a)  Kwa kutumia vyanzo mbalimbali, sikiliza wimbo wa bongo fleva unaosawiri

                   umuhimu wa elimu, kisha jibu maswali yafuatayo:
                   (i)  Ni dhamira zipi zinazopatikana katika wimbo huu?

                   (ii)  Ni maadili gani unayoyapata kutokana na wimbo huu?
                   (iii)  Ni imani zipi zinazodhihirika katika wimbo huu?

                   (iv)  Kuna uhusiano gani kati ya maadili yaliyoelezwa na imani za jamii
                        yako?

              (b)  Tumia vyanzo vya mtandaoni au vinginevyo kusikiliza wimbo wa bongo

                   fleva, kisha linganisha maadili yaliyomo na imani za jamii.
              Ulinganisho wa maadili na imani katika ushairi
              Ushairi ni utanzu muhimu katika  jamii  kwani waandishi wengi wamekuwa
              wakitunga  mashairi  yenye malengo  ya kufunza, kuonya na kuadibu. Ushairi
              hupata uhai wake kutokana na hali halisi za kijamii, ikiwa ni pamoja na imani
              na maadili ya jamii husika. Hii inamaanisha kwamba utanzu huu hubeba maadili
              yanayoendana na imani zilizomo katika jamii.

               Shughuli ya 4.7
              (a) Soma shairi lifuatalo, kisha linganisha maadili yaliyomo na imani za jamii

                  kwa kujibu maswali yanayofuata.



                          Mchwa na Kumbikumbi
                          Nchi yetu kichuguu, ndani yake tunaishi,

                          Tumbo letu na miguu, vyote ndani vinaishi,

                          Mawazo yetu kwa Mungu, aliyeweka utashi,
                          Kwa nini mwatunyanyasa, wakati wote twaishi?






                     Kitabu cha Mwanafunzi                                            99
                        Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   99                    23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   99
   105   106   107   108   109   110   111   112   113   114   115