Page 109 - Fasihi_Kisw_F5
P. 109

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                                    kijana tu akatoweka. Alifahamu kuwa baba yake mdogo
                                    atatuandikia.  (Anaita  tena). Huka...Nikija  huko, kweli
                                    nitakuchapa. Afadhali uje mwenyewe.

                                           Huka (Ngahyoma, 1973)
          FOR ONLINE READING ONLY
                   Maswali


                   (i)  Ni dhamira zipi zinazopatikana katika matini hii?

                   (ii)  Ni kwa namna gani matukio katika matini hii yanafumbata maadili?
                   (iii)  Matendo ya wahusika yanasawiri maadili? Kwa nini?

                   (iv)  Ni kwa namna gani lugha iliyotumiwa na wahusika inaakisi maadili?
                        (toa sababu)

                   (v)  Ni matukio gani katika matini hii hayaakisi maadili ya jamii yako?

              (b)  Chambua maadili yanayopatikana katika tamthiliya mbili teule ulizosoma.

              (c)  Angalia au sikiliza tamthiliya mbili zinazorushwa katika vituo vya runinga
                   au redio, kisha chambua maadili yanayopatikana katika tamthiliya hizo.

               Shughuli ya 4.5
              Kwa kutumia  vyanzo mbalimbali,  chambua  kazi  nne za ushairi na nne za
              tamthiliya, kisha bainisha masuala ya kiimani yaliyomo katika kazi hizo.



              Ulinganisho wa maadili yaliyomo katika kazi za fasihi na imani za
              jamii
              Imani ni hali ya mtu kukubali jambo fulani kuwa ni kweli na anapaswa
              kuliheshimu. Aghalabu,  imani  hujielekeza  katika  masuala  ya  dini.  Miongoni
              mwa maudhui yanayowasilishwa  kwenye kazi  za  fasihi hutokana  na imani
              iliyomo katika jamii. Hivyo kuna uhusiano mkubwa baina ya maadili na imani.
              Dhana hizi hujengana na kuathiriana kiasi kwamba wakati mwingine ni vigumu
              kuvitenganisha. Ieleweke kuwa wakati mwingine kuna imani ambazo huweza
              kumsukuma au kumwelekeza mtu kufanya matendo yasiyo na maadili. Kutokana
              na uwasilishwaji wa masuala mbalimbali, ni muhimu kuzingatia imani za jamii
              husika katika uchambuzi  wa maadili  yanayojitokeza katika  kazi  za kifasihi.
              Ulinganisho wa maadili katika imani unaweza kuangaliwa katika kazi za kifasihi
              kama vile bongo fleva, mashairi na tamthiliya.




                98                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   98
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   98                    23/06/2024   17:54
   104   105   106   107   108   109   110   111   112   113   114