Page 69 - Fasihi_Kisw_F5
P. 69

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Mchango wa fasihi simulizi katika maendeleo ya fasihi andishi
              Maendeleo  ya fasihi andishi kabla ya uhuru yana uhusiano mkubwa na
              wamisionari na watawala wa kigeni. Wageni hawa walipofika pwani ya Afrika
              Mashariki, waliwakuta  wenyeji wakiwa na fasihi yao. Kwa mfano, baadhi
          FOR ONLINE READING ONLY
              ya tenzi za zamani  kama vile  Fumo Liyongo  zilikuwa zikisimuliwa  kabla ya
              maandishi na ziliwekwa katika maandishi baadaye. Pia, tenzi hizi zilitokana na
              nyimbo ambazo ndizo fasihi ya awali.

              Halikadhalika, kuna athari za mashairi na fani nyinginezo kama tarihi, masimulizi
              ya wasafiri, ngano na hekaya mbalimbali. Ngano na hekaya hizi ndizo zilitafsiriwa
              na kuwa msingi wa hadithi za awali za Kiswahili. Miongoni mwa hadithi hizo
              ni Swahili Tales as Told by the Natives of Zanzibar (1870) zilizotafsiriwa na
              Edward Steere. Ngano nyingine zimechapishwa katika Kitabu cha Prosa und
              Poesie der Suaheli (1907) kilichohaririwa na Carl Velten, Mazungumzo ya Alfu
              Lela Ulela Juzuu (1-4) (1928) kilichotafsiriwa na Edwin Brenn na kuhaririwa na
              Frederick Johnson na Hekaya za Abunuwasi (Chiponde, 1928). Kisiwa chenye
              Hazina (Johnson, 1929), Safari za Gulliver (Swift, 1932), Mashimo ya Mfalme
              Suleimani (Haggard, 1937) na Safari ya Msafiri (Bunyan, 1925).

              Kama ulivyojifunza  kuhusu tanzu na vipera vya fasihi simulizi, fasihi hii
              inajumuisha hadithi, semi, ushairi na sanaa za maonesho na vipera vyake. Baadhi
              ya tanzu hizi hujitokeza katika fasihi andishi kwani vipengele mbalimbali vya
              tanzu hizo huweza kutumika kama mbinu za kisanaa katika kazi za fasihi andishi.
              Mfano wa vipengele hivyo ni wahusika wasio binadamu kama vile wanyama,
              mashetani na mazimwi, kama wanavyojitokeza katika riwaya za vitisho na za
              kingano. (Senkoro, 2011).

              Kuanzia miaka ya 1940 hadi 1960, riwaya nyingi za Kiswahili zilifuata mkondo
              wa hekaya  na ngano. Kimaudhui,  riwaya  hizo  zilielezea  mambo  ya mila  na
              desturi kama njia ya kutunza maadili. Mifano ya riwaya hizo ni Adili na Nduguze
              (Robert, 1952), Kusadikika (Robert, 1991) na Kufikirika (Robert, 1968).


              Kimsingi, fasihi simulizi imekuwa nguzo ya fasihi andishi katika kueneza
              tamaduni mbalimbali za kijamii. Waandishi mbalimbali wamechota fikra kutoka
              katika kazi mbalimbali za kifasihi simulizi na kuzitumia katika tungo za fasihi
              andishi.

               Shughuli ya 2.17
              Chunguza vipindi vya fasihi simulizi  vinavyorushwa na vituo vya runinga
              au sikiliza  vipindi  kutoka katika  vituo  viwili  vya redio,  kisha eleza  athari
              zinazotokana na vipindi hivyo kurushwa kwa njia hizo.


                58                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   58
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   58                    23/06/2024   17:54
   64   65   66   67   68   69   70   71   72   73   74