Page 71 - Fasihi_Kisw_F5
P. 71

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




              Matumizi ya simu nayo yana mchango mkubwa katika jamii. Watu wengi hutumia
              simu kwa mawasiliano ya mazungumzo. Kuwapo kwa mawasiliano ya mitandao
              ya kijamii kwa kutumia simu kumewezesha uwasilishaji na uenezaji wa fasihi
              simulizi. Baadhi ya simu zina uwezo wa kurekodi na kutuma nyimbo, masimulizi
              na picha. Pia, zina uwezo wa kunasa vituo mbalimbali vya redio na runinga na,
          FOR ONLINE READING ONLY
              hivyo, kuwawezesha watumiaji wake kusikiliza kazi za kifasihi. Vilevile, vifaa
              kama vile vishikwambi, na kompyuta vimerahisisha uhifadhi, ubebaji, na usomaji
              wa kazi za fasihi andishi. Zaidi, teknolojia imesaidia kupatikana kwa majukwaa ya
              kidijiti kama vile mitandao ya kijamii ambayo watunzi wa kazi za fasihi simulizi
              na andishi huitumia kuwasilishia au kuuzia kazi zao.

              Kadhalika, kutokana na maendeleo ya kiteknolojia, fasihi simulizi pia imekuwa
              ikiwasilishwa kwa njia ya maandishi. Hii inatokana na kuongezeka kwa viwanda
              vya uchapaji ambavyo vimerahisisha mchakato wa uzalishaji wa machapisho ya
              kazi mbalimbali za fasihi, zikiwamo zinazotokana na fasihi simulizi.

               Shughuli ya 2.18
              (a)  Kusanya semi kumi (10) za Kiswahili kulingana na makundi yafuatayo:
                   (i)  Methali tano (5) zinazoonya kuhusu utovu wa nidhamu.

                   (ii)  Misemo mitano (5) inayohamasisha umoja na ushirikiano katika jamii.

              (b)  Jadili mchango wa semi ulizozikusanya na umuhimu wake kwa maendeleo
                   ya jamii.


              Mchango wa fasihi simulizi na fasihi andishi katika maendeleo ya jamii
              Fasihi  simulizi  na andishi  zimekuwa  na mchango  mkubwa kwa jamii  ambao
              umesaidia  katika  kuigeuza  na kuibadilisha  jamii.  Mchango huo umeweza
              kujidhihirisha kama ifuatavyo:

              (a)  Kuelimisha jamii
              Mchango  mkubwa wa fasihi  simulizi  na  andishi  ni  kuelimisha  jamii.  Fasihi
              huufumbua macho umma na kupiga vita matatizo ya njaa, maradhi, umaskini na
              mengineyo. Aidha, fasihi huipa jamii maarifa na stadi za kukabiliana na mazingira
              ambamo jamii inaishi. Kwa mfano, kuna nyimbo mbalimbali zinazotoa elimu juu
              ya utunzaji wa mazingira. Kutokana na nyimbo hizo jamii imeweza kuelimika na
              kupata maarifa ya namna ya kutunza mazingira pamoja na kuendeleza shughuli za
              maendeleo binafsi na ya kitaifa. Jamii inasisitiza kuwa mazingira yasipotunzwa
              husababisha mabadiliko hasi ya tabia nchi.







                60                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   60
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   60                    23/06/2024   17:54
   66   67   68   69   70   71   72   73   74   75   76