Page 125 - Fasihi_Kisw_F5
P. 125

Fasihi ya Kiswahili  kwa Shule za Sekondari




                   Avita:    Usiniambie!

                   Vera:      Ndo  nakwambia  sasa.  Isitoshe,  wasomi  wengi  wana  migogoro
                            isiyo na suluhu ya ndoa. Wake zao wasomi wana mambo hamsini
                            kidogo. Mara wanaandika paper, mara vikao, mara appointment za
          FOR ONLINE READING ONLY
                            mheshimiwa. Kwa kupenda au kutokupenda, kujua au kutokujua,
                            wanajikuta wanawaacha wanaume zao wakiwa na njaa, hapo ndo
                            wanatuachia njia nyeupeee. Kufa kufaana.


                   Avita:   [Anaangua kicheko cha nguvu]. Yaani wewe umepinda, hapo ndo
                            nakupendea mtu wangu.

                   Beti:    Yaani mnavunja ndoa za watu halafu  mnapongezana?  Mh!
                            Wonders will never end

                            [Anapiga makofi na kubetua mdomo kuonesha mshangao]

                   Vera:      Point of correction, hatuvunji, kimsingi tunawasaidia kuondoa
                            stress zao.


                              Wakiingia kwenye mihadhara  wapoleee. Fikiria wangekuja na
                            stress kwenye  kumbi  za  mihadhara,  si ingekuwa  kimbembe.
                            Yaani, watu kama sisi ni wa muhimu kwa maendeleo ya taifa.

                   Beti:    Nawahurumia, hamjui mlifanyalo, halafu mnaongea kwa sauti na
                            kujiamini. Akina mama wakitokea hapa, hamwogopi?


                                    Halahala (Mbijima, 2019: 52 - 53)

                   Maswali

                   (i)  Imani na mitazamo gani inajitokeza katika matini hii?

                   (ii)  Mitazamo ya mwandishi kuhusu mwanamke ina athari gani katika
                        jamii?

                   (iii)   “Nina wengine, siyo mwingine. Kwa uzuri huu wanaonitaka ni wengi,
                        lazima nibadili ladha.” Kauli hii inaweza kuleta athari gani kwa vijana?
                   (iv)  Unafikiri mitazamo iliyomo katika matini hii ina uhalisi wowote katika
                        jamii? Kwa nini?






               114                                                 Kitabu cha Mwanafunzi
                                                                     Kidato cha Tano



                                                                                            23/06/2024   17:54
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   114
     FASIHI YA KISWAHILI KITABU CHA MWANAFUNZI KIDATO CHA TANO.indd   114                   23/06/2024   17:54
   120   121   122   123   124   125   126   127   128   129   130