Page 6 - Historiayatznamaadili
P. 6

Utangulizi





              Kitabu cha Historia ya Tanzania na Maadili kimeandikwa
          FOR ONLINE READING ONLY
              mahususi kwa ajili ya mwanafunzi wa Darasa la Nne, Tanzania
              Bara. Kitabu hiki kimeandaliwa kulingana na muhtasari wa somo

              la Historia ya Tanzania na Maadili uliotolewa na Wizara ya Elimu,
              Sayansi na Teknolojia mwaka 2023.


              Kitabu hiki kina sura nane, nazo ni: Wajibu na haki za mtoto
              katika jamii na Taifa, Maendeleo ya jamii kabla ya ukoloni,
              Sayansi na teknolojia za asili kabla ya ukoloni, Shughuli za
              uchumi kabla ya ukoloni, Ushirikiano na uhusiano wa kijamii
              na kiuchumi, Mamlaka za jadi kabla ya ukoloni, Mamlaka za

              jadi katika ukuzaji na utunzaji wa maadili, na Alama za Taifa
              na utambullisho wa Taifa. Maudhui ya kitabu cha Historia ya
              Tanzania na Maadili Darasa la Nne yamejikita zaidi katika historia

              ya Tanzania na maadili na watu wake kabla ya ukoloni. Kwa
              kujifunza maudhui ya kitabu hiki, mwanafunzi atamudu historia
              ya Tanzania na maadili yake kabla ya ukoloni. Aidha, maudhui
              haya yatamwezesha kumudu maarifa, stadi na mwelekeo wa
              kuwa mzalendo, kujenga maadili, kukuza utaifa na kulinda

              rasilimali anuwai za Taifa zilizojengwa kwa vipindi tofauti nchini.
              Hivyo, kumwezesha kuishi katika misingi ya utu, uadilifu, umoja,
              upendo, amani na kuthamini rasilimali za Taifa na watu wake

              pasipokujali rangi, dini,  jinsi zao, wala mahali wanapotoka.

              Maudhui ya sura hizi yamewasilishwa kwa njia ya matini, kazi za
              vitendo, picha zenye mvuto na mazoezi. Kwa hiyo, mwanafunzi

              anapaswa kufanya mazoezi na kazi zote zilizopo kwenye kitabu
              hiki pamoja na kazi nyingine atakazopewa na mwalimu ili kufikia
              lengo la somo la Historia ya Tanzania na Maadili kwa Darasa
              la Nne.





                                                    v




                                                                                          06/11/2024   11:29:24
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   5
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   5                                      06/11/2024   11:29:24
   1   2   3   4   5   6   7   8   9   10   11