Page 8 - Historiayatznamaadili
P. 8

Sura ya          Wajibu na haki za mtoto


                   Kwanza               katika jamii na Taifa


          FOR ONLINE READING ONLY


                   Utangulizi


                Wajibu na haki za mtoto ni muhimu kwa maendeleo ya mtoto katika jamii
                na Taifa. Ulipokuwa Darasa la Tatu, ulijifunza kuhusu wajibu na haki za
                mtoto shuleni na nyumbani. Katika sura hii, utajifunza kuhusu wajibu na

                haki za mtoto katika jamii na Taifa. Umahiri utakaoupata utakuwezesha
                kutambua wajibu na haki za mtoto katika jamii na Taifa. Hivyo, kukuwezesha
                kutekeleza wajibu wako ili kurahisisha kupata haki zako katika jamii na

                Taifa kwa ujumla.



                            Fikiri


                             Wajibu na haki za mtoto katika jamii na Taifa.



              Dhana ya wajibu na haki za mtoto


                                Kazi ya kufanya namba 1

                           Soma matini kutoka vyanzo mbalimbali, ikiwamo

                           maktaba mtandao kuhusu wajibu na haki za mtoto
                           katika jamii na Taifa.



              Wajibu ni mambo ya lazima ambayo mtu hupaswa kuyatenda
              ili kukabili mazingira yanayomzunguka. Wajibu huambatana
              na sheria za jamii na Taifa ambazo ni lazima kuzitekeleza na
              kuzitimiza. Hii ina maana usipotimiza wajibu, utaonekana kuwa

              mtu wa tofauti. Ibara ya 25-28 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano
              wa Tanzania inaeleza kuhusu wajibu wa Watanzania wote na



                                                    1




                                                                                          06/11/2024   11:29:25
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   1                                      06/11/2024   11:29:25
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   1
   3   4   5   6   7   8   9   10   11   12   13