Page 12 - Historiayatznamaadili
P. 12

Kazi ya kufanya namba 3


                           Jadili na andika matendo yanayoashiria mtoto
                           kuheshimiwa, kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake
          FOR ONLINE READING ONLY
                           katika jamii.




              Kulindwa na kupata haki sawa

              Kila mtoto ana haki ya kulindwa dhidi ya mateso, vitisho na
              kupewa adhabu zinazomdhalilisha. Kimsingi, haki hii inahusu

              ulinzi wa mtoto dhidi ya ukatili, unyanyasaji, uonevu na udhalilishaji
              wa aina yoyote katika jamii yake na Taifa.  Vyombo vya ulinzi
              kuanzia ngazi za Mtaa/Kijiji, Kata hadi Taifa vimewekwa kwa ajili
              ya ulinzi na usalama wa mtoto. Aidha, endapo mtoto atafanyiwa

              vitendo vya ukatili, unyanyasaji, uonevu na udhalilishaji, ana
              wajibu wa kutoa taarifa katika vyombo vya usalama ili kupata
              msaada.


                                Kazi ya kufanya namba 4

                           Chunguza na andika zilipo ofisi za Mtaa/Kijiji, Kata

                           na Taifa maeneo yanayokuzunguka ambapo mtoto
                           anaweza kutoa taarifa iwapo haki zake zitakiukwa.




              Kusikilizwa kwa ukamilifu

              Mtoto ana haki ya kushiriki na kujadili masuala yanayomhusu
              katika mikutano na vikao katika jamii inayomzunguka. Hivyo, ana
              haki ya kutoa mawazo yake bila kuathiri sheria za nchi katika

              jamii na Taifa. Haki hii humpa mtoto nafasi ya kushiriki katika
              kutoa uamuzi wa masuala yanayohusu ustawi wake. Mtoto ni
              raia kama walivyo raia wengine katika serikali ya Jamhuri ya
              Muungano wa Tanzania.





                                                    5




                                                                                          06/11/2024   11:29:28
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   5
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   5                                      06/11/2024   11:29:28
   7   8   9   10   11   12   13   14   15   16   17