Page 15 - Historiayatznamaadili
P. 15

Kimsingi, watoto wana wajibu wa kutekeleza katika jamii na
              Taifa. Sheria ya mtoto na Katiba vinaeleza wajibu wa mtoto
              katika familia, jamii na Taifa. Hii ni kwa sababu mtoto ni sehemu
              ya jamii na Taifa. Kielelezo namba 3, kinaonesha watoto wenye
          FOR ONLINE READING ONLY
              mabango yenye baadhi ya wajibu wa mtoto.





























                      Kielelezo namba 3: Wajibu wa mtoto katika jamii na Taifa


              Kupenda kufanya kazi
              Mtoto ana wajibu wa kufanya kazi katika jamii na Taifa kulingana
              na umri na uwezo wake. Mtoto anapofanya kazi hujenga
              mshikamano na jamii na Taifa lake. Pia, humfanya mtoto
              kukubalika katika jamii yake. Jamii zote hukemea uvivu na
              kutokupenda kufanya kazi. Hivyo, ni wajibu wa mtoto kupenda
              na kufanya kazi ili kuwa na tabia zinazokubalika katika jamii
              na Taifa. Kielelezo namba 4, kinaonesha watoto wakishiriki
              kusafisha mazingira katika jamii.


                                Kazi ya kufanya namba 8

                           Fanya uchunguzi, kisha andika kazi ambazo mtoto

                           anaweza kushiriki katika jamii inayomzunguka.





                                                    8




                                                                                          06/11/2024   11:29:29
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   8                                      06/11/2024   11:29:29
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   8
   10   11   12   13   14   15   16   17   18   19   20