Page 18 - Historiayatznamaadili
P. 18

Kuonesha heshima na utii katika jamii

              Mtoto ana wajibu wa kuheshimu watu waliomzidi umri, pamoja
              na watoto wenzake bila ya kujali rangi, hali ya maisha au jinsi.
              Heshima inaweza kuoneshwa kwa kusalimia watu wengine,
          FOR ONLINE READING ONLY
              kukubali kutumwa na kufanya kazi bila kuonesha kiburi. Pia,

              mtoto anaweza kuonesha heshima kwa kuwasaidia wazee,
              watu wenye mahitaji maalumu na watu wengine katika jamii
              yake na Taifa kwa ujumla. Aidha, mtoto kuonesha unyenyekevu
              na kukubali kuelekezwa katika mambo halali na ya msingi ni
              sehemu ya kuonesha heshima na utii katika jamii. Wajibu huu ni

              muhimu kwa mtoto ili kukubalika katika jamii. Licha ya kuonesha
              heshima kwa watu wengine, mtoto ana wajibu wa kujiheshimu.


                                Kazi ya kufanya namba 11

                             Jadili na orodhesha matendo yanayoonesha

                             kujiheshimu na ya kutojiheshimu katika jamii
                             inayokuzunguka.



              Matendo ya kujiheshimu kwa mtoto ni yale yanayokubalika na

              jamii yake. Matendo ya kutojiheshimu ni yale yasiyokubalika
              na jamii yake. Mtoto hapaswi kuiga na kutenda matendo yaliyo
              kinyume na maadili ya jamii na Taifa lake. Pia, mtoto ana wajibu

              wa kukubali na kufuata kanuni na sheria ambazo jamii imejiwekea
              ili kuishi salama katika jamii yake.


                      Zoezi namba 2


                1.  Eleza umuhimu wa mtoto kujiheshimu katika jamii yake.

                2.  Je, kuna umuhimu gani wa mtoto kuwaheshimu watu
                      wengine katika jamii?








                                                   11




                                                                                          06/11/2024   11:29:31
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   11
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   11                                     06/11/2024   11:29:31
   13   14   15   16   17   18   19   20   21   22   23