Page 22 - Historiayatznamaadili
P. 22

jamii moja na nyingine. Hivyo, ni wajibu wa mtoto kujifunza
              mambo mema ya utamaduni wa jamii yake na Taifa lake, ili
              kuishi kulingana na mahitaji ya jamii yake na Taifa lake.

                                Kazi ya kufanya namba 15
          FOR ONLINE READING ONLY

                             Waulize wazazi au walezi kuhusu mila na desturi
                             za jamii yako, kisha andika wajibu wako katika

                             kuzitekeleza.


              Kimsingi, mtoto ana wajibu wa kujifunza na kuendeleza
              utamaduni wa jamii inayomzunguka. Hivyo, mtoto anapaswa

              kujifunza utamaduni wa jamii yake kutoka kwa wazazi, walezi na
              watu wengine katika jamii. Aidha, mtoto ana wajibu wa kujifunza
              na kuheshimu mila na desturi zinazoendeleza amani, utulivu,
              utu na heshima.


              Kujilinda na kujijali
              Mtoto anao wajibu wa kujilinda na kujijali. Kujilinda ni kujikinga
              dhidi ya mazingira hatarishi kwa kuepuka kuwa katika maeneo

              hatarishi.  Mfano,  kutokutembea  usiku,  kutokwenda  katika
              vilabu vya pombe au magenge ya wavuta bangi na dawa za
              kulevya. Mtoto hapaswi kuangalia picha chafu kwenye mitandao
              ya kijamii au kujihusisha katika urafiki wa kimapenzi akiwa na
              umri mdogo. Mtoto anatakiwa kuwa katika maeneo salama na
              kuepuka maeneo ya uficho na kujitenga na watoto wengine.
              Pia, mtoto hapaswi kuiga vitendo viliyo kinyume na maadili ya
              jamii na Taifa lake.


                                Kazi ya kufanya namba 16


                             Jadili namna mtoto anavyoweza  kujilinda na
                             kujijali katika mazingira yake.









                                                   15




                                                                                          06/11/2024   11:29:34
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   15
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   15                                     06/11/2024   11:29:34
   17   18   19   20   21   22   23   24   25   26   27