Page 24 - Historiayatznamaadili
P. 24

FOR ONLINE READING ONLY




















                         Kielelezo namba 7: Watoto wakishiriki kupinga rushwa

                                Kazi ya kufanya namba 17


                        Orodhesha miradi ya maendeleo inayotekelezwa na
                        serikali, kisha:

                        1. Andika faida ya jamii kushiriki katika kuzuia vitendo
                           vya rushwa katika miradi hiyo.

                        2. Andika madhara ya vitendo vya rushwa katika miradi

                           hiyo.


              Kushirikiana na watoto wengine katika jamii na Taifa

              Watoto ndio tegemeo la jamii na Taifa. Hivyo, ni wajibu wa
              mtoto kushirikiana na watoto wengine katika jamii na Taifa ili
              kujenga misingi ya maendeleo ya jamii zao. Ushirikiano na
              watoto wengine katika jamii na Taifa huwajengea uwezekano

              wa kufanya kazi pamoja sasa na baadaye. Pia, hujenga umoja
              wa watoto kitaifa. Hivyo, ni wajibu wa watoto, kushirikiana na
              watoto wengine ili kujenga uhusiano na umoja kati yao kwa
              maendeleo ya jamii na Taifa.



                                                   17




                                                                                          06/11/2024   11:29:34
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   17
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   17                                     06/11/2024   11:29:34
   19   20   21   22   23   24   25   26   27   28   29