Page 25 - Historiayatznamaadili
P. 25

Kazi ya kufanya namba 18


                             Jadili namna mtoto anavyoweza kushirikiana na
                             watoto wengine katika jamii na Taifa.
          FOR ONLINE READING ONLY

              Wajibu huu wa mtoto, umeambatana na sheria, hivyo, mtu
              anapokiuka wajibu anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria.

                                Kazi ya kufanya namba 19


                             Jadili mambo uliyojifunza kuhusu wajibu wa mtoto
                             katika jamii na Taifa.


              Umuhimu wa wajibu na haki za mtoto katika jamii na Taifa


                                Kazi ya kufanya namba 20

                             Jadili umuhimu wa haki na wajibu wa mtoto katika
                             jamii na Taifa.



              Wajibu na haki za mtoto ni muhimu kwa mtoto binafsi, jamii na
              Taifa. Haki na wajibu wa mtoto ni muhimu kwani husaidia kuleta
              ulinzi, heshima na fursa kwa watoto katika jamii na Taifa. Pia,
              mtoto anayetambua haki na wajibu wake, hutekeleza wajibu
              wake, na hudai haki zake. Hivyo, kumwezesha kupata haki zake

              katika jamii na Taifa. Aidha, jamii inayotambua haki na wajibu
              wa mtoto inaweza kumsaidia mtoto kutimiza wajibu wake. Hivyo,
              kupata haki zake.  Kwa ujumla haki na wajibu humsaidia mtoto:

              (a)  Kujikinga dhidi ya ukatili, unyanyasaji na udhalilishaji
                    kwa mtoto; Mtoto anayetambua haki zake katika jamii na
                    Taifa ni rahisi kufahamu vitendo vilivyo kinyume na haki

                    zake.  Hivyo, kuchukua hatua za kujilinda kwa kudai haki
                    zake. Pia, huweza kutoa taarifa katika vyombo na mamlaka
                    zinazohusika au mashirika yanayoshughulikia masuala

                    ya watoto. Vilevile, anaweza kuwasaidia watoto wenzake



                                                   18




                                                                                          06/11/2024   11:29:34
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   18
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   18                                     06/11/2024   11:29:34
   20   21   22   23   24   25   26   27   28   29   30