Page 26 - Historiayatznamaadili
P. 26

kutambua haki zao kama watoto. Kimsingi, hii humsaidia
                    mtoto kujilinda na ukatili, unyanyasaji na udhalilishaji dhidi
                    ya watoto.

              (b)  Kujitambua na kuchukua hatua stahiki za usalama;
          FOR ONLINE READING ONLY
                    Mtoto anayefahamu haki zake, huweza kujitetea katika

                    mazingira yanayomzunguka. Pia, huweza kujisimamia dhidi
                    ya vitendo vya unyanyasaji, udhalilishaji na ukatili katika
                    jamii.  Aidha, mtoto anayetekeleza wajibu wake, huweza
                    kuishi maisha salama na kupata fursa mbalimbali katika

                    jamii na Taifa.

              (c)  Kujenga uhusiano katika jamii na Taifa; Mtoto anayejua
                    haki zake na kutekeleza wajibu wake, ni rahisi kujenga
                    uhusiano mwema na kushirikiana na watu wengine katika
                    jamii na Taifa. Kwa mfano, mtoto anayejua haki ni rahisi
                    kushiriki katika mijadala ya kijamii na kisiasa kuhusu

                    masuala yanayohusu watoto. Hivyo, humwezesha kujenga
                    uhusiano na watu wengine katika jamii na Taifa.

              (d)  Kuwa raia mwema; Mtoto anayefahamu haki zake na
                    wajibu wake, ni rahisi kuwa raia mwema katika jamii na
                    Taifa. Utekelezaji wa haki na wajibu wa mtoto katika jamii

                    na Taifa, huwezesha watoto kujitambua na kuishi katika
                    misingi ya maadili, haki na usawa katika jamii.

              (e)  Kujenga maadili; Kujua haki zake, humsaidia mtoto
                    kutenda vitendo vyenye maadili. Pia, humwezesha kufanya
                    uamuzi wenye maadili kuhusu tabia zake na kutambua

                    jinsi ya kuwatendea mema watu wengine.

              (f)  Kuimarisha ustawi wake katika jamii na Taifa; Mtoto
                    kufahamu haki zake na kutekeleza wajibu wake, huimarisha
                    ustawi wake kijamii na kitaifa.  Haki na wajibu wa mtoto
                    huongeza ushiriki wa mtoto katika shughuli za kijamii na

                    Taifa. Hivyo, humwezesha kuimarisha usalama na ulinzi
                    wa mtoto.


                                                   19




                                                                                          06/11/2024   11:29:34
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   19                                     06/11/2024   11:29:34
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   19
   21   22   23   24   25   26   27   28   29   30   31