Page 31 - Historiayatznamaadili
P. 31

Kazi ya kufanya namba 3


                           Jadili mambo yanayoashiria maendeleo ya jamii.


          FOR ONLINE READING ONLY
              Maendeleo ya jamii hutafsiriwa kwa kuangalia uwezo wa
              wanajamii wa kuyakabili mazingira yao. Pia, huangaliwa katika
              uwezo wa jamii wa kujipatia mahitaji yake, kujitegemea na
              kusimamia mipango ya maendeleo. Vilevile, huangaliwa katika
              uwezo wa kutumia rasilimali zilizopo katika mazingira kama
              vile rasilimali watu, vitu, fedha, ardhi, pamoja na sayansi na
              teknolojia ya jamii katika kutatua changamoto zao. Maendeleo
              hayapaswi kuangaliwa kwa kulinganisha jamii moja na nyingine
              tu, kwani jamii hutofautiana katika rasilimali walizonazo.


              Umuhimu wa maendeleo ya jamii

              Maendeleo ya jamii ni muhimu kwa ustawi wa mtu binafsi,
              jamii na Taifa. Mfano, maendeleo katika elimu husaidia kukuza
              maarifa na ujuzi wa jamii katika utendaji wa kazi. Aidha, elimu
              huongeza ufanisi katika shughuli za uchumi na maendeleo
              ya jamii. Maendeleo katika afya huboresha afya ya jamii, kwa

              maana ya kukinga na kuponya jamii na magonjwa. Maendeleo
              katika afya huwezesha kuwa na jamii yenye afya njema na
              inayoshiriki kikamilifu katika kuleta maendeleo ya jamii na Taifa.
              Vivyo hivyo, maendeleo katika miundombinu kama vile barabara,
              miradi ya maji na umeme huongeza fursa za kiuchumi. Pia,
              makazi bora husaidia jamii kuwa na mahali salama pa kuishi na
              huiwezesha jamii kufanya kazi za kujiletea maendeleo binafsi
              na ya Taifa. Kimsingi, maendeleo ya jamii ni msingi wa ustawi
              wa jamii inayohusika.


              Maendeleo ya jamii kabla ya ukoloni
              Kabla ya kuja kwa wakoloni, jamii za Kitanzania zilikuwa na
              maendeleo kadhaa katika afya, elimu na makazi. Maendeleo
              hayo yaliwezesha watu kupata huduma za afya, elimu na kuishi

              katika makazi bora.


                                                   24




                                                                                          06/11/2024   11:29:36
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   24
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   24                                     06/11/2024   11:29:36
   26   27   28   29   30   31   32   33   34   35   36