Page 33 - Historiayatznamaadili
P. 33

mzazi alikuwa mwalimu wa kwanza wa mtoto. Watu walijifunza
              wakati wote katika mazingira yanayowazunguka ili kuwawezesha
              kuyakabili mazingira yao. Hivyo, jamii za wakulima zilijifunza
              kilimo, jamii za wavuvi zilijifunza uvuvi. Vivyo hivyo, jamii za
          FOR ONLINE READING ONLY
              wahunzi na wafugaji. Vijana walifunzwa pia majira ya mwaka;
              kiangazi na masika. Watu walifundishwa kazi zilizofanywa katika
              majira haya. Kimsingi, elimu kabla ya wakoloni ilifundisha watu
              kujitegemea na kuyakabili mazingira yao.


              Pia, vijana hasa wa kiume, walipofikia umri fulani walipewa
              mafunzo ya ulinzi ili kulinda jamii zao. Vijana walifundishwa
              kutengeneza silaha; kama vile pinde, mishale, mikuki na sime.
              Aidha, kila mwanajamii aliandaliwa vizuri na alikuwa tayari

              kulinda jamii yake. Kielelezo namba 2, kinaonesha vijana wakiwa
              na silaha za asili za ulinzi.





































                    Kielelezo namba 2: Vijana wakiwa na silaha za asili za ulinzi






                                                   26




                                                                                          06/11/2024   11:29:38
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   26
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   26                                     06/11/2024   11:29:38
   28   29   30   31   32   33   34   35   36   37   38