Page 32 - Historiayatznamaadili
P. 32

Kazi ya kufanya namba 4

                           Soma matini mbalimbali kuhusu maana ya neno

                           ukoloni.
          FOR ONLINE READING ONLY

              Nchi yetu kwa nyakati tofauti, imetawaliwa na wageni kutoka

              nchi za Ulaya. Mfano wa wageni hao ni kutoka katika nchi
              za Ujerumani na Uingereza. Wageni hao walipokuja nchini
              waliondoa utawala na mamlaka zilizokuwapo katika jamii zetu,
              kisha kututawala kiuchumi, kisiasa na kijamii. Huo ukawa ndio

              mwanzo wa utawala wa kikoloni nchini.

                                Kazi ya kufanya namba 5


                           Waulize wazazi au walezi kuhusu maendeleo ya jamii
                           yaliyokuwapo katika jamii yenu kabla ya ukoloni.




              Maendeleo ya jamii katika elimu kabla ya ukoloni
              Jamii zetu zilikuwa na maendeleo katika elimu, ingawa mfumo
              wa elimu uliokuwapo, ulikuwa tofauti na huu tulionao sasa. Watu

              hawakwenda shule na kuingia darasani kusoma, kuandika na
              kuhesabu kama ilivyo sasa.


                                Kazi ya kufanya namba 6

                           Waulize wazazi au walezi kuhusu aina ya elimu
                           iliyotolewa katika jamii inayowazunguka kabla ya
                           ukoloni.



              Elimu kabla ya ukoloni ilitolewa kulingana na shughuli za jamii
              na mazingira yaliyoizunguka. Vijana na watoto walifundishwa
              maarifa na stadi kama vile kilimo, uvuvi, uhunzi, ususi, upishi,

              ufugaji na kadhalika.  Elimu hii ilikuwa na shabaha ya kuwaandaa
              watoto na vijana kwa maisha halisi katika jamii zao.  Hivyo,



                                                   25




                                                                                          06/11/2024   11:29:36
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   25
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   25                                     06/11/2024   11:29:36
   27   28   29   30   31   32   33   34   35   36   37