Page 29 - Historiayatznamaadili
P. 29

Sura ya               Maendeleo ya jamii


                        Pili                kabla ya ukoloni


          FOR ONLINE READING ONLY


                   Utangulizi


                Maendeleo ni jambo muhimu katika maisha ya jamii. Katika sura hii,
                utajifunza kuhusu maendeleo ya jamii za Kitanzania kabla ya ukoloni.
                Utajifunza kuhusu maendeleo ya jamii katika elimu, afya na makazi.

                Umahiri utakaoupata, utakusaidia kutambua maendeleo ya jamii za
                Kitanzania kabla ya ukoloni. Hivyo, kuthamini na kuendeleza maendeleo
                hayo katika jamii zetu kwa sasa.




                            Fikiri


                             Maendeleo ya jamii nchini kabla ya ukoloni.





              Dhana ya maendeleo


                                Kazi ya kufanya namba 1

                           Soma vyanzo mbalimbali, ikiwamo maktaba
                           mtandao kuhusu maana ya neno “maendeleo”.





              Maendeleo ni hali ya ongezeko au kupiga hatua fulani. Pia,
              maendeleo huhusisha ukuaji. Ukuaji huo unaweza kuwa ni
              kutoka hatua moja ya chini kwenda nyingine. Kielelezo namba 1,
              kinaonesha mtoto anapanda ngazi kutoka hatua ya chini kwenda
              ya juu, na kila apandapo anaongeza hatua.







                                                   22




                                                                                          06/11/2024   11:29:35
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   22
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   22                                     06/11/2024   11:29:35
   24   25   26   27   28   29   30   31   32   33   34