Page 30 - Historiayatznamaadili
P. 30

FOR ONLINE READING ONLY





















                      Kielelezo namba 1:  Mtoto akipanda hatua za maendeleo
              Pia, maendeleo hutafsiriwa kwa kuangalia ongezeko katika idadi

              kutoka idadi ndogo kwenda idadi kubwa. Mfano, tunapokuwa
              shuleni, tumekuwa tukiongeza maarifa na stadi fulani siku hadi
              siku. Huu ni mfano wa maendeleo katika ujifunzaji.

              Viashirio vya maendeleo ya jamii

                                Kazi ya kufanya namba 2


                           Soma matini mbalimbali, ikiwamo maktaba mtandao
                           kuhusu viashirio vya maendeleo.



              Viashirio vya maendeleo vinaweza kuonekana katika mabadiliko
              yanayotokea kutoka hatua moja kwenda nyingine. Mfano,
              mabadiliko katika ongezeko la vitu na mali. Pia, yanaweza kuwa
              katika ujuzi na maarifa aliyonayo mtu na jinsi anavyoyatumia
              katika kutatua changamoto anazokutana nazo. Maendeleo

              yanaweza kuwa kwa mtu binafsi, jamii au Taifa kwa ujumla.
              Maendeleo kwa mtu binafsi yapo katika mabadiliko ya ongezeko
              la vitu, mali na hata maarifa na stadi katika maisha yake.



                                                   23




                                                                                          06/11/2024   11:29:36
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   23
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   23                                     06/11/2024   11:29:36
   25   26   27   28   29   30   31   32   33   34   35