Page 37 - Historiayatznamaadili
P. 37

Zoezi namba 1


                1.  Bainisha mambo muhimu yaliyozingatiwa katika elimu
                      kabla ya ukoloni.
          FOR ONLINE READING ONLY
                2.  Fafanua njia zilizotumika katika utoaji wa elimu kabla
                      ya ukoloni.

                3.  Bainisha tofauti zilizokuwapo katika utoaji wa elimu kabla
                      ya ukoloni na sasa.


              Elimu ilitolewa kwa kuzingatia rika na jinsi. Kwa mfano, kulikuwa
              na elimu kwa vijana wa kiume wakati wa balehe iliyojulikana
              kama “Elimu ya Jando”. Pia, ilikuwapo elimu kwa vijana wa
              kike iliyojulikana kama “Elimu ya Unyago”.  Elimu hii ilikuwa na

              manufaa sana katika jamii zetu.  Vijana walifundishwa kuhusu
              mabadiliko ya ukuaji katika miili yao na majukumu yao kwa jamii na
              familia.  Pia, walifundishwa kuhusu maadili ya jamii zao.


              Maendeleo ya makazi ya jamii kabla ya ukoloni
              Makazi ya jamii kabla ya ukoloni ni mahali ambapo jamii za kale
              ziliishi. Jamii zetu kabla ya ukoloni zilikuwa na makazi kama

              ilivyosasa.

                                Kazi ya kufanya namba 8

                           Waulize wazazi au walezi kuhusu:

                             1.  Nyumba zilizojengwa na jamii yenu.

                             2.  Mambo yaliyozingatiwa katika ujenzi wa makazi
                                 ya jamii yenu.


              Makazi ya jamii za kale yalitegemeana na mazingira ya eneo,
              shughuli za kiuchumi, malighafi za ujenzi zilizopo na maendeleo
              ya jamii inayohusika. Jiografia ya eneo, pia ilikuwa jambo muhimu
              katika jamii kuamua eneo na aina ya makazi.  Mambo haya

              yalizingatiwa ili jamii iweze kuishi katika mazingira salama na
              rafiki kwa maisha yao. Mfano, jamii nyingi zilijenga makazi katika


                                                   30




                                                                                          06/11/2024   11:29:40
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   30
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   30                                     06/11/2024   11:29:40
   32   33   34   35   36   37   38   39   40   41   42