Page 38 - Historiayatznamaadili
P. 38

maeneo ya karibu na vyanzo vya maji ili kupata maji na samaki.
              Pia, zilijenga kandokando ya milima ili kufanya shughuli za kilimo
              na kukwepa mafuriko. Aidha, jamii za kale ziliepuka ujenzi katika
              maeneo yenye wanyama wakali, yenye magonjwa, tetemeko la
          FOR ONLINE READING ONLY
              ardhi, mafuriko na vimbunga.

              Aina za makazi kabla ya ukoloni
              Jamii za kale zilikuwa na makazi ya aina mbalimbali. Aidha,

              tofauti za ujenzi wa makazi hayo, ziliakisi malighafi za ujenzi
              zilizopatikana katika mazingira ya jamii inayohusika. Mfano,
              ujenzi ulifuata uwepo wa nyasi, mianzi, matete, miti mirefu
              na mifupi, udongo na makuti. Pia, ujenzi wa nyumba hizo,
              ulitegemea utamaduni wa jamii na ukubwa wa familia, kama
              vile idadi ya watoto na wake katika familia. Mfano, jamii za
              Wangoni na Wanyakyusa zilijenga nyumba kubwa na ndogo eneo

              moja. Nyumba kubwa ilitumika kwa ajili ya wazazi na watoto
              wadogo na ile ndogo kwa ajili ya vijana wa kiume. Wahehe
              walijenga nyumba kubwa iliyokuwa na vyumba vingi kwa sababu
              familia ziliishi pamoja. Wamasai walijenga nyumba kama boma
              kulingana na idadi ya wake na watoto.  Wachaga, Wahaya,
              Wanyambo na Wasukuma walijenga nyumba mbili katika eneo
              lao. Nyumba moja ilikuwa kwa ajili ya kulala watu na nyumba
              nyingine kwa ajili ya kulala mifugo, kupikia na kuhifadhia mazao.
              Baadhi ya jamii zilijenga nyumba moja, ambamo walitenga eneo

              la kukaa watu na kulaza wanyama.

                                Kazi ya kufanya namba 9


                           Andika mambo uliyojifunza kuhusu ujenzi wa makazi
                           ya jamii kabla ya ukoloni ukilinganisha na ya sasa.




              Muundo wa ujenzi wa makazi ya jamii za Kitanzania ulikuwa wa
              aina tatu ambazo ni msonge, tembe na banda.







                                                   31




                                                                                          06/11/2024   11:29:41
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   31
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   31                                     06/11/2024   11:29:41
   33   34   35   36   37   38   39   40   41   42   43