Page 43 - Historiayatznamaadili
P. 43

Nyumba za tembe
              Nyumba za tembe zilijengwa kwa kutumia miti iliyosukwa kwa
              kamba na fito, kisha kukandikwa kwa udongo ili ziwe imara.
              Nyumba hizi hushikiliwa na nguzo imara. Nyumba za tembe
          FOR ONLINE READING ONLY
              huezekwa nyasi na miti, kisha kukandikwa kwa udongo juu.
              Nyumba hizi zilikuwa fupi na zenye umbo la mstatili. Nyumba za
              tembe zilijengwa na jamii zilizoishi mkoa wa Dodoma, Singida
              na Manyara. Dodoma zilijengwa na jamii za Wagogo, Singida
              na jamii za Wanyaturu na Wanyiramba na Manyara na jamii za
              Wairaqw. Kielelezo namba 12, 13 na 14, vinaonesha mfano wa
              nyumba za tembe.






















              Kielelezo namba 12:  Nyumba ya tembe iliyojengwa kwa miti chini na
                                      kufunikwa kwa udongo juu























                  Kielelezo namba 13:  Nyumba ya tembe ya jamii za Wagogo na
                           Wanyaturu iliyojengwa kwa udongo juu na chini

                                                   36




                                                                                          06/11/2024   11:29:46
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   36
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   36                                     06/11/2024   11:29:46
   38   39   40   41   42   43   44   45   46   47   48