Page 47 - Historiayatznamaadili
P. 47

Umuhimu wa maendeleo ya jamii kabla ya ukoloni

              Maendeleo ya jamii kabla ya ukoloni, yalisaidia uendelezaji wa
              shughuli za uchumi na jamii.  Mfano, maendeleo ya jamii katika
              elimu yalikuwa chanzo cha kuboresha maarifa na ujuzi wa jamii.
          FOR ONLINE READING ONLY
              Hivyo, kuongeza maarifa na ujuzi katika uzalishaji. Maendeleo

              katika huduma za afya yaliboresha ustawi wa jamii, kwa jamii
              kuwa na watu wenye afya njema katika ushiriki wa shughuli
              za kijamii na kiuchumi. Vivyo hivyo, maendeleo katika makazi
              yalisababisha jamii kuwa na mahali salama pa kuishi.



                        Zoezi la jumla

               1.  Andika NDIYO kwa sentensi iliyo kweli na HAPANA kwa

                     sentensi isiyo kweli.

                    (i)  Maendeleo yaliyopo katika jamii zetu yaliletwa na
                         wakoloni _____________

                    (ii)  Makazi ya jamii za kale yalitegemea shughuli za uchumi
                         na jiografia ya eneo linalohusika ________________

                    (iii)  Mbinu ya vitendo ilitumika zaidi kufundishia na
                         kujifunzia kabla ya ukoloni____________

                    (iv)  Jamii za kale tayari zilikuwa na dawa za kutibu
                         magonjwa mbalimbali katika jamii kabla ya ukoloni
                         ________________

                    (v)  Jamii zetu zilikuwa na maendeleo katika elimu, ingawa
                         mfumo wa kutoa elimu ulikuwa tofauti na huu tulionao
                         sasa____________

               2.  Taja mambo muhimu yaliyozingatiwa katika ujenzi wa
                     makazi kabla ya ukoloni.

               3.  Fafanua faida za elimu kabla ya ukoloni kwa maendeleo
                     ya jamii.

               4.  Eleza mbinu zilizotumika kutibu jamii kabla ya ukoloni.




                                                   40




                                                                                          06/11/2024   11:29:48
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   40
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   40                                     06/11/2024   11:29:48
   42   43   44   45   46   47   48   49   50   51   52