Page 51 - Historiayatznamaadili
P. 51

FOR ONLINE READING ONLY


































                Kielelezo namba 1: Utengenezaji wa zana, Zama za Mawe za Kale


              Zana hizi zilimsaidia mwanadamu kuongeza mawindo na
              chakula zaidi, kwani aliweza kuchimba mizizi mingi zaidi kwa
              muda mfupi na kuua wanyama wadogo kwa ajili ya kitoweo.

              Pia, zana hizo zilimsaidia kujihami na wanyama wakali. Vilevile,
              zilitumika kuchunia ngozi za wanyama na kukata nyama. Aidha,
              mawe yenye ncha kali yalitumika kukatia mizizi iliyotumika

              kama chakula na dawa. Pia, yalitumika kutenganisha mizoga
              ya wanyama ili kuwa rahisi kuibeba. Sayansi na teknolojia za
              utengenezaji wa zana za mawe zilileta maendeleo makubwa
              katika maisha ya binadamu kulingana na mahitaji ya jamii ya
              wakati huo. Kielelezo namba 2, kinaonesha maumbo ya baadhi

              ya zana za Zama za Mawe za Kale.


                                                   44




                                                                                          06/11/2024   11:29:50
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   44
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   44                                     06/11/2024   11:29:50
   46   47   48   49   50   51   52   53   54   55   56