Page 46 - Historiayatznamaadili
P. 46

Jamii za kale kabla ya ukoloni, zilitumia tiba za asili. Tiba hizo
              zilitokana na mitishamba kama vile majani, mizizi, magamba
              na magome ya miti. Pia, mafuta, ngozi na manyoya ya baadhi
              ya wanyama vilitumika kama dawa. Dawa zilitumika kutibu kwa
          FOR ONLINE READING ONLY
              kunywa, kupaka, kufukiza, kuoga au kunusa.  Kulikuwa na watu
              rasmi waliokuwa na ujuzi na maarifa ya kutibu magonjwa kwa
              kutumia dawa za asili. Mtu alipougua alipelekwa kwa mganga
              kwa ajili ya matibabu na alipata huduma za tiba kama ilivyo

              sasa. Ushauri wa tiba ulitolewa na wataalamu wa tiba wa jamii.
              Mfano, kuna magonjwa ambayo mgonjwa alitakiwa kupumzika
              na hata kula aina za vyakula kama tiba. Pia, tiba hizi zilihusisha
              mazoezi mbalimbali katika mwili wakati wa matibabu.


              Aidha, palikuwapo na huduma za afya ya uzazi ambazo zilitolewa
              tangu pale kijana alipobalehe ili kumpa maarifa na stadi kwa ajili
              ya uzazi bora. Vijana wa kike walifundishwa afya ya uzazi kuanzia

              malezi ya mimba mpaka kujifungua mtoto. Pia, walifundishwa
              chakula kinachofaa na jinsi ya kujilinda wakati wa ujauzito. Hii
              ilifanyika ili kuwawezesha kupata uzazi bora na salama. Aidha,

              palikuwa na watu rasmi waliohusika na shughuli za ukunga
              katika jamii. Elimu ya afya ya uzazi ilisaidia uzazi salama na
              kuepuka magonjwa yanayosababisha ukosefu wa uzazi.


              Jamii za kale zilizingatia ulaji wa chakula bora kama sehemu ya
              tiba. Matumizi ya dawa za asili na ulaji wa chakula bora, vilifanya
              jamii za kale kuwa na afya imara. Afya ya jamii ilikuwa jambo la
              kuzingatiwa sana katika jamii za kale.



                                Kazi ya kufanya namba 14

                           Andika mambo uliyojifunza kuhusu maendeleo ya
                           afya ya jamii kabla ya ukoloni.









                                                   39




                                                                                          06/11/2024   11:29:48
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   39                                     06/11/2024   11:29:48
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   39
   41   42   43   44   45   46   47   48   49   50   51