Page 49 - Historiayatznamaadili
P. 49

Sura ya         Sayansi na teknolojia za


                       Tatu            asili kabla ya ukoloni


          FOR ONLINE READING ONLY
                   Utangulizi



                Sayansi na teknolojia za asili zilikuwa na mchango mkubwa katika
                maendeleo ya jamii kabla ya kuja kwa ukoloni. Katika sura hii, utajifunza
                sayansi na teknolojia za asili kuhusu utengenezaji wa zana za mawe,
                chuma na chumvi. Pia utajifunza kuhusu sayansi na teknolojia asilia za tiba

                za asili, kilimo, uvuvi, ufinyanzi, ususi na uchongaji na maadili yake. Vilevile,
                utajifunza michango ya sayansi na teknolojia hizo katika maendeleo ya jamii
                na uchumi. Umahiri huu, utakuwezesha kuthamini sayansi na teknolojia
                za asili kabla ya ukoloni na maadili yake. Hivyo, kutumia maarifa na ujuzi

                huu katika kuendeleza shughuli za uchumi na jamii kwa sasa.


                            Fikiri


                             Sayansi na teknolojia ya asili katika jamii za
                             Kitanzania kabla ya ukoloni.


              Dhana ya sayansi na teknolojia za asili

              Sayansi  na  teknolojia  za  asili  zinajumuisha  matumizi  ya
              maarifa na ujuzi asilia wa wenyeji katika kuyakabili mazingira
              yanayowazunguka. Maarifa na ujuzi ambao ulitokana na
              utamaduni, rasilimali asilia, watu na vitu. Sayansi na teknolojia

              asilia zilihusisha uvumbuzi, ubunifu  na kufanya majaribio katika
              kutengeneza zana na vifaa mbalimbali kwa lengo la kuyakabili
              mazingira, kutatua matatizo, kurahisisha na kuboresha utendaji

              wa shughuli katika jamii. Msingi wa sayansi na teknolojia asilia
              ulikuwa kutafuta suluhisho la changamoto katika kukidhi mahitaji
              ya jamii. Aidha, sayansi na teknolojia asilia ziliendelea kukua
              kulingana na uhitaji wa jamii, mazingira na nyakati zilizohusika.



                                                   42




                                                                                          06/11/2024   11:29:49
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   42
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   42                                     06/11/2024   11:29:49
   44   45   46   47   48   49   50   51   52   53   54