Page 53 - Historiayatznamaadili
P. 53

Kazi ya kufanya namba 2

                           Chunguza zana katika kielelezo namba 2 na 3, kisha

                           andika tofauti ya zana za Zama za Mawe za Kale
                           na za Kati.
          FOR ONLINE READING ONLY


              Pia, binadamu alianza kutengeneza nguo kwa kutumia ngozi
              za wanyama. Sayansi na teknolojia ya utengenezaji nguo kwa
              kutumia ngozi za wanyama ilifanywa kwa kuloanisha ngozi za

              wanyama na kuzipondaponda ili ziwe laini, kisha kutengeneza
              nguo. Aidha, katika Zama za Mawe za Kati binadamu aligundua
              moto.


              Sayansi na teknolojia ya asili ya kutengeneza moto
              Sayansi na teknolojia ya kutengeneza moto iligundulika katika
              harakati za utengenezaji wa zana, ambapo binadamu aligundua

              uwapo wa cheche za moto wakati akigongagonga na kusugua
              mawe.  Pia, binadamu aliona cheche za moto zilizotokana na
              radi, wakati radi ilipopiga. Hii ilisababisha binadamu kufanya
              majaribio zaidi ya utengenezaji wa moto. Binadamu alianza kwa

              kupekecha vijiti viwili vikavu ili kupata moto. Kielelezo namba 4,
              kinaonesha sayansi na teknolojia ya awali ya kutengeneza moto.

























              Kielelezo namba 4: Sayansi na teknolojia ya asili ya kutengeneza moto


                                                   46




                                                                                          06/11/2024   11:29:51
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   46
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   46                                     06/11/2024   11:29:51
   48   49   50   51   52   53   54   55   56   57   58