Page 56 - Historiayatznamaadili
P. 56
binadamu. Sayansi na teknolojia asilia ya Zama za Mawe
iliboreshwa katika kila nyakati. Hivyo, kuboresha uwezo wa
mwanadamu wa kupambana na mazingira na maisha yake.
Kwa mfano:
FOR ONLINE READING ONLY
(a) Ugunduzi wa zana katika Zama za Mawe za Kale,
uliimarisha shughuli za uwindaji kwa kuongeza mazao
ya uwindaji;
(b) Zana za mawe kipindi cha Zama za Mawe za Kati zilikuwa
bora zaidi, nyepesi na zilitumika kwa ajili ya kufanyia
kazi mahususi. Zana hizo zilitumika katika uwindaji na
kutengenezea nguo zilizotokana na ngozi za wanyama.
Pia, ugunduzi wa moto katika Zama za Mawe za Kati
ulileta maendeleo katika matumizi ya chakula. Aidha,
binadamu alitumia moto kuzuia baridi, hivyo, alianza
kuishi katika mapango; na
(c) Zana za Zama za Mawe za Mwisho, zilileta maendeleo
zaidi katika shughuli za uvuvi na uwindaji. Zana hizo
zilimwezesha binadamu kuwinda wanyama zaidi na
kuvua samaki kwa urahisi ikilinganishwa na hapo awali.
Pia, zilitumika katika kilimo.
Baadhi ya viashirio vya kuanza kwa shughuli za kilimo na ufugaji
mwishoni mwa Zama za Mawe za Mwisho ni:
(i) Kuanza kwa shughuli za kilimo za kuotesha au
kupanda mazao ya chakula na shughuli za ufugaji
wa wanyama wadogo. Hivyo, binadamu kupata
chakula cha kutosha;
(ii) Binadamu kuanza kuishi katika makazi ya kudumu
kwa ajili ya shughuli za kilimo na ufugaji; na
(iii) Kuibuka kwa uhitaji wa uongozi katika jamii. Pia,
huu ulikuwa mwanzo wa mgawanyo wa kazi baina
ya jinsi (kike na kiume) na marika (watoto, vijana
na wazee).
49
06/11/2024 11:29:52
Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd 49
Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd 49 06/11/2024 11:29:52