Page 60 - Historiayatznamaadili
P. 60

kuwinda  na  kujilinda  dhidi  ya  wanyama  wakali  na  maadui.
              Zana zingine za chuma ni mundu, ambayo ilitumika kwa ajili ya
              kufyeka na kusafisha maeneo kwa ajili ya kilimo. Vilevile, chuma
              kilitumika kutengenezea visu kwa ajili ya kuchunia wanyama na
          FOR ONLINE READING ONLY
              kukatia nyama. Majembe yalitumika kulimia na kuchimbia mizizi
              na wanyama wafukuao ardhi.

              Baadhi ya zana za chuma ziliwekewa mipini ili kurahisisha

              matumizi yake. Zana za chuma zilileta mapinduzi makubwa
              katika sayansi na teknolojia asilia hasa katika kilimo, uwindaji,
              ulinzi na uvuvi kabla ya ukoloni. Kielelezo namba 9, kinaonesha

              zana za chuma zenye mpini.

























                       Kielelezo namba 9: Zana za chuma zilizowekwa mpini

              Baadhi ya jamii zilizojishughulisha na uzalishaji wa chuma ni
              Wanyambo, Wahaya, Wazinza, Wafipa, Wapare, Wasambaa,

              Wayao, Wangoni, Wahehe, Warongo na Wanyamwezi.

                                Kazi ya kufanya namba 3


                           Onesha katika ramani maeneo yalipo makabila
                           yaliyojishughulisha na ufuaji wa chuma.







                                                   53




                                                                                          06/11/2024   11:29:54
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   53
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   53                                     06/11/2024   11:29:54
   55   56   57   58   59   60   61   62   63   64   65