Page 65 - Historiayatznamaadili
P. 65

hawakuruhusiwa kulima katika maeneo yenye vyanzo vya maji
              na katika mifereji. Maeneo yaliyofanya kilimo cha umwagiliaji,
              palikuwapo na kanuni za kutumia maji kwa ajili ya umwagiliaji.
              Kwa mfano, watu waliruhusiwa kutiririsha maji katika mashamba
          FOR ONLINE READING ONLY
              yao kwa zamu. Pia, maji haya yalitumika kipindi cha ukame
              tu. Hii ilifanyika kwa lengo la kuwezesha uhifadhi wa maji na
              mgawanyo wa maji kwa watu wote. Pia, kilimo cha mazao
              mchanganyiko kilifanyika ili kuhifadhi ardhi isichoke haraka.

              Maadili haya yalisaidia uhifadhi wa ardhi na kuwa na maji kwa
              ajili ya kilimo kipindi cha ukame. Sayansi na teknolojia hizo
              zilisaidia kuongeza mazao ya kilimo.

                                Kazi ya kufanya namba 6


                            Jadili mambo uliyojifunza kuhusu maadili katika
                            sayansi  na  teknolojia  za  kilimo  na  jinsi  ya
                            kuziendeleza katika kilimo kwa sasa.



                      Zoezi namba 2


                1.  Andika  sayansi  na  teknolojia  za  asili  katika  kilimo
                      zilizotumika nchini kabla ya ukoloni.

                2.  Eleza maadili yaliyoambatana na shughuli za kilimo
                      kabla ya ukoloni.

                3.  Eleza umuhimu wa kutumia teknolojia asilia za kilimo
                      na maadili yake kwa jamii zetu kwa sasa.


              Sayansi na teknolojia asilia katika ufugaji


                                Kazi ya kufanya namba 7

                           Fanya uchunguzi kuhusu shughuli za ufugaji
                           zinazofanyika katika maeneo yanayokuzunguka.








                                                   58




                                                                                          06/11/2024   11:29:55
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   58                                     06/11/2024   11:29:55
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   58
   60   61   62   63   64   65   66   67   68   69   70