Page 67 - Historiayatznamaadili
P. 67

Kazi ya kufanya namba 8

                           Andika mambo uliyojifunza kuhusu sayansi na

                           teknolojia ya ufugaji na jinsi ya kuyaendeleza kwa
                           sasa.
          FOR ONLINE READING ONLY


              Sayansi na teknolojia za asili katika uvuvi

              Sayansi na teknolojia asilia katika uvuvi ilitumia vifaa kama vile
              ndoano, ngalawa, mitumbwi na mitego ya asili. Ndoano hizo
              zilitengenezwa na jamii za wahunzi kwa kutumia chuma. Wavuvi

              waliweka chambo mbalimbali katika ndoano ili kuvutia samaki
              kwa lengo la kuwatega. Wavuvi waliweza kuwavua samaki
              pindi walipokula chambo kwenye ndoano. Kielelezo namba 12,

              kinaonesha uvuvi kwa kutumia ndoano.





























                           Kielelezo namba 12: Uvuvi kwa kutumia ndoano


              Pia, uvuvi ulifanyika kwa kutumia nyavu za asili zilizosukwa.
              Wavuvi walitupa nyavu katika kina kirefu cha maji mengi ili
              kuvua samaki. Samaki walipopita katika eneo walilotupa nyavu

              walinaswa. Matumizi ya ngalawa na mitumbwi yalisaidia wavuvi



                                                   60




                                                                                          06/11/2024   11:29:56
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   60
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   60                                     06/11/2024   11:29:56
   62   63   64   65   66   67   68   69   70   71   72