Page 68 - Historiayatznamaadili
P. 68

kwenda mbali kwenye maji yenye kina kirefu. Kielelezo namba
              13, kinaonesha uvuvi kwa kutumia nyavu.




          FOR ONLINE READING ONLY

























                           Kielelezo namba 13: Uvuvi kwa kutumia nyavu

              Vilevile, wavuvi walitumia mitego ya samaki kama vile madema
              ambayo yalitokana na sayansi na teknolojia ya ususi. Sayansi
              na teknolojia hizi ziliwawezesha wavuvi kuvua samaki wengi.

              Uhifadhi wa samaki ulifanywa kwa kutumia chumvi na moto. Hii
              ilisaidia kuwa na samaki kwa matumizi ya baadaye na kwa ajili
              ya biashara.


              Shughuli za uvuvi zilifanyika zaidi na jamii zilizoishi maeneo ya
              maziwa, mito na katika sehemu za Pwani ya Bahari ya Hindi.

              Jamii zilizoishi maeneo ya mwambao wa bahari na ziwa, ndizo
              zilizojishughulisha zaidi na uvuvi. Mfano katika Pwani ya Bahari
              ya Hindi na Visiwa vya Zanzibar, jamii zilizojihusisha na uvuvi
              ni Wamakua, Wadigo, Watumbatu, Wandengereko, Wamwera
              na Wakojani. Ukanda wa Ziwa Viktoria walikuwa Wakerewe,

              Wajita, Wasukuma, Wakwaya, Wakara na Wajaluo. Ukanda
              wa Ziwa Tanganyika ni Waha, na ukanda wa Ziwa Nyasa ni
              Wanyasa na Wakisi.


                                                   61




                                                                                          06/11/2024   11:29:57
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   61
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   61                                     06/11/2024   11:29:57
   63   64   65   66   67   68   69   70   71   72   73