Page 72 - Historiayatznamaadili
P. 72

kuhifadhia maji na nafaka. Aidha, vyombo hivi vilitumika katika
              kubadilishana ili kupata bidhaa zilizokosekana katika jamii ya
              wafinyanzi.
                                Kazi ya kufanya namba 10
          FOR ONLINE READING ONLY
                           Jadili namna ya kuendeleza sayansi na teknolojia ya

                           ufinyanzi katika jamii zetu kwa maendeleo ya sasa.




              Sayansi na teknolojia asilia ya ususi
              Sayansi na teknolojia ya ususi ilifanywa kwa kutumia malighafi

              kama vile ukindu, mianzi, matete, miwaa na majani ya minazi
              na michikichi. Ususi ulifanywa kwa kusuka kitu. Mfano, makuti

              ya minazi au chikichi yalisukwa kwa kutumia mikono au ukindu.
              Ukindu ulitengenezwa kutokana na chale za minazi au michikichi.
              Sayansi na teknolojia ya ususi ilifanyika kwa kupishanisha kindu,

              mianzi, matete au majani ya minazi na michikichi kwa mpangilio
              maalumu ili kupata umbo fulani. Kielelezo namba 19, kinaonesha
              mfano wa kitanda kilichosukwa kwa makuti na kamba.


























                  Kielelezo namba 19: Kitanda kilichosukwa kwa kamba za ukili na
                                                 makuti

              Sayansi na teknolojia ya ususi kwa kutumia mianzi ilifanywa
              kwa kutumia mianzi ambayo ilivunwa na kuchunwa kitaalamu,


                                                   65




                                                                                          06/11/2024   11:30:01
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   65
     Historia ya Tanzania na Maadili STD IV.indd   65                                     06/11/2024   11:30:01
   67   68   69   70   71   72   73   74   75   76   77